عن عبد الله بن عباس رضي الله عنه قال: «شَهِد عِندِي رِجَال مَرْضِيُون - وأَرْضَاهُم عِندِي عُمر- أنَّ النَبِي صلى الله عليه وسلم نَهَى عن الصَّلاة بَعد الصُّبح حتَّى تَطلُعَ الشَّمسُ، وبعد العصر حتَّى تَغرُب». وعن أبي سعيد رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم أنه قال: «لا صَلاَة بعد الصُّبح حتَّى تَرتَفِعَ الشَّمسُ، ولا صَلاَة بعد العَصرِ حتَّى تَغِيبَ الشَّمس».
[صحيح] - [حديث ابن عباس رضي الله عنه: متفق عليه. حديث أبي سعيد رضي الله عنه: متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdallah bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: "Walishuhudia kwangu wanaume wanaoridhiwa -na ninaye mridhia zaidi kwangu ni Omar- yakwamba Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amekataza kuswali baada ya swala ya sub-hi mpaka lichomoze jua, na baada ya laasiri mpaka lizame" Na kutoka kwa Abuu Saidi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- yakwamba yeye amesema: "Hakuna swala baada ya sub-hi mpaka linyanyuke jua, na wala hakuna swala baada ya laasiri mpaka litoweke jua".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy na Muslim kwa riwaya zake

Ufafanuzi

Amekataza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hizi mbili kuswali baada ya swala ya sub-hi mpaka lichomoze jua na linyanyuke toka msitari wa mawingu katika mtazamo wa macho kwa kiasi cha urefu wa mshale, na hili linaweza kukadiriwa kwa dakika kadhaa, wametofautiana wanachuoni katika kiwango chake, kuanzia dakika tano (5) mpaka kumi na tano (15). Na amekataza pia kuswali baada ya swala ya laasiri mpaka litoweke jua, kabla ya adhana ya magharibi kwa dakika chache; kwasababu katika kuswali ndani ya nyakati hizi kuna kujifananisha na washirikina wale wanaoliabudu wakati wa kuchomoza kwake na kuzama kwake, na tumekatazwa kujifananisha nao katika ibada zao; kwasababu atakayejifananisha na watu fulani basi nayeye ni miongoni mwao.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama