عن أبي قتادة الأنصاري رضي الله عنه مرفوعاً: "لا يُمْسِكَنَّ أَحَدُكُم ذَكَره بَيمِينِه وهو يبول، ولا يَتَمَسَّحْ من الخلاء بيمينه، ولا يَتَنَفَّس في الإناء".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Qatada Al-Answariy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Asishike mmoja wenu utupu wake kwa mkono wake wa kulia akiwa anakidhi haja ndogo, na asijifute haja ndogo au kubwa kwa mkono wake wa kulia na asipumulie ndani ya chombo anachonywea".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Anamuamrisha Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- muislamu asishike utupu wake wakati wa haja ndogo, na asiondoe najisi kutoka mbele au nyuma kwa mkono wake wa kulia, na anakataza pia kupumulia katika chombo anachonywea kwasababu ya madhara mengi yaliyoko katika hilo.