عن أبي بشير الأنصاري رضي الله عنه "أنه كان مع رسول الله صلى الله عليه وسلم في بعض أسفاره، فأرسل رسولا أن لا يَبْقَيَنَّ في رقبة بَعِيرٍ قِلادَةٌ من وَتَرٍ (أو قلادة) إلا قطعت".
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Bashir Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-"Yakwamba yeye alikuwa pamoja na Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake katika baadhi ya safari zake, akatuma mjumbe asibakishe katika shingo ya mnyama chochote kinachotundikwa ispokuwa kikatwe".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Nikuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake alituma katika baadhi ya safari zake mwenye kutangaza kwa watu kuondoa vinavyotundikwa ambavyo viko katika shingo za ngamia ambavyo lengo lake ni kuzuia kijicho na kuzuia maafa, kwasababu hilo ni katika shirki ambayo ni lazima kuiondoa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa kutundika kamba za upinde -kwaajili ya kuzuia maafa- ni haramu, na inazingatiwa kuwa ni katika kutundika hirizi.
  2. Kuwafikishia watu yale yanayolinda itikadi yao.
  3. Uwajibu wa kukemea uovu kwa kadiri ya uwezo.
  4. kukubalika habari ya mtu mmoja.
  5. Kubatilishwa kwa itikadi za manufaa yanayotokana na kamba ya aina yoyote ile.
  6. Naibu wa kiongozi anasimamia nafasi ya kiongozi katika yale aliyokabidhiwa.
  7. Inampasa kiongozi wa watu awe mwenye kuchunga hali zao, awakague na atazame katika hali zao.
  8. Na ni wajibu kwa kiongozi wa watu kuwachunga kwa mujibu wa sheria, wakifanya mambo ya haramu anawazuia, na wakizembea katika wajibu anawahimiza juu yake.
Ziada