عن مَرْثَد الغَنَويّ رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم أنه قال:«لا تصلُّوا إلى القُبُور، ولا تجلِسُوا عليها».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Marthadi Al-Ghanawiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- yakwamba yeye Amesema: "Msiswali makaburini, wala msiyakalie makaburi".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Amekataza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuswali katika makaburi, yaani kaburi liwe upande wa mwenye kuswali, na vile vile amekataza kukaa juu ya makaburi, na katika hilo ni kuyadhalilisha kwa kuyakanyaga kwa miguu, au kukidhi haja juu yake, na yote hayo ni haramu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Katazo la kuswali katika makaburi, yaani kaburi liwe upande wa mwenye kuswali, na katazo linamaanisha kuharibika kwa kile kilichokatazwa.
  2. Kufunga milango yote inayopelekea katika ushirikina.
  3. Katazo la kukaa juu ya makaburi; kwasababu ndani yake kuna aina fulani ya kumdhalilisha mwenye kaburi.
  4. Kukusanya kati ya katazo la kuchupa mipaka katika makaburi, na kutoyadhalilisha; na hii ni kwasababu kuswali katika makaburi kunapelekea kulitukuza kaburi na kuchupa mpaka ndani yake, na kukaa kunapelekea kulidhalilisha, ukakataza uislamu kuchupa mipaka ndani yake na kulidhalilisha, tusilipuuze wala tusichupe mipaka.
  5. Nikuwa heshima ya maiti muislamu hubakia baada ya kufa kwake, na linatiliwa nguvu hili na kauli yake Rehema na Amani ziwe juu yake-: (Kuvunja mfupa wa maiti ni kama kuuvunja akiwa hai). Na linazalika katika hili: Kuwa hao wanaowadhalilisha maiti kwa kukata viungo vyao baada ya vifo vyao hakika wamekosea; kwasababu hii ni aina ya kumdhalilisha maiti, na ni kumuadhibu, na kwasababu hii wametoa ushahidi wanachuoni kuwa ni haramu kukata kiungo cha maiti hata kama alitoa usia wa hilo, kwasababu yeye hana maamuzi tena katika nafsi yake.
  6. Haifai kuegemea juu ya kaburi na huku sio kukaa, lakini ikiwa watu wanalichukulia hilo kimazoea kuwa ni udhalilishaji basi haitakiwi kuliegemea; kwasababu kinachozingatiwa ni muonekano, madamu muonekano unahesabika kimazoea kuwa ni kudhalilisha, basi hilo hata kama ni halali kulifanya ni wajibu kuliepuka.
Ziada