عن عائشة رضي الله عنها ، قالت: سَأَل رسول الله صلى الله عليه وسلم أُنَاسٌ عن الكُهَّان، فقال: «ليْسُوا بشيء» فقالوا: يا رسول الله إنهم يُحَدِّثُونَا أحْيَانَا بشيء، فيكون حَقَّا؟ فقال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «تلك الكلمة من الحَقِّ يخْطفُها الجِنِّي فَيَقُرُّهَا في أُذُنِ وليِّه، فَيَخْلِطُونَ معها مائة كَذِبَة».
وفي رواية للبخاري عن عائشة رضي الله عنها : أنها سمعت رسول الله صلى الله عليه وسلم يقول: «إن الملائكة تَنْزِل في العَنَانِ -وهو السَّحَاب- فَتَذْكُرُ الأمر قُضِيَ في السماء، فَيَسْتَرِقُ الشيطان السَّمْعَ، فيسمعه، فيُوحِيَه إلى الكُهَّان، فيكذبون معها مائة كَذْبَة من عند أَنْفُسِهم».
[صحيح] - [الرواية الأولى: متفق عليها.
الرواية الثانية: رواها البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-, Amesema: walimuuliza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake watu kuhusu makuhani, Akasema: "Si lolote" Wakasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, hutusimulia wakati mwingine jambo na likatokea kweli, Akasema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake: "Neno hilo ni katika maneno ya kweli anayoibia jini na akalinong'oneza katika sikio la bwana wake, kisha wakachanganya pamoja na neno hilo uongo mia moja". Na katika riwaya ya Bukhariy- kutoka kwa Aisha Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba yeye alimsikia Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake Akisema: "Hakika Malaika huteremka katika mawingu- wakalitaja jambo lililopitishwa mbinguni, basi shetani huiba kusikia, na akalisikia, kisha akaliteremsha kwa makuhani kisha wanaongopa pamoja na neno hilo uongo mia moja toka kwao wenyewe".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Anaeleza Aisha Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba watu walimuuliza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kuhusu wale wanaosimulia kuhusu mambo ya ghaibu yajayo, akasema: Msiwajali wala msiyachukue maneno yao wala haliwahusu jambo lao. Wakasema: Hakika kauli yao huendana na ukweli, kama ambavyo wanaweza kuelezea kutokea kwa jambo katika mwezi fulani na siku fulani, na likatokea kwa kuendana na kauli yao, Akasema Rehema na Amani ziwe juu yake- Hakika majini huibia wanayoyasikia katika habari za mbinguni, kisha wanateremka kwa mabwana zao katika makuhani wakawaeleza yale waliyoyasikia, kisha anaongeza huyu kuhani katika haya aliyoyasikia kutoka mbinguni uongo mia moja. Na maana ya riwaya ya Bukhariy: Nikuwa Malaika husikia mbinguni yale anayoyapitisha Mwenyezi Mungu Mtukufu kila siku katika matukio kwa watu wa duniani, kisha wanashuka katika mawingu, wakahadithiana baadhi yao kwa baadhi, wakaibia mashetani habari hizo, kisha wakateremka nazo kwa mabwana zao katika makuhani wakawaeleza yale waliyoyasikia, kisha kuhani huongeza katika yale aliyoyasikia uongo mia moja au zaidi.