عن ابن عمر رضي الله عنهما:
أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ نَهَى عَنِ الْقَزَعِ.

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 5921]
المزيــد ...

Kutoka kwa bin Omari -Radhi za Allah ziwe juu yao yeye na baba yake-:
Yakuwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amekataza kunyoa kiduku.

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake] - [Swahiih Al Bukhaariy - 5921]

Ufafanuzi

Amekataza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kunyoa baadhi ya nywele za kichwa na kuacha baadhi.
Na katazo linawahusu watu wote, mwanaume mtoto mdogo na mkubwa pia, ama mwanamke hatakiwi kunyoa nywele za kichwa chake.

Katika Faida za Hadithi

  1. Sheria ya Uislamu imetilia umuhimu wa muonekano wa kibinadamu.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (62)