عن أنس رضي الله عنه قال:
كُنَّا عِنْدَ عُمَرَ فَقَالَ: «نُهِينَا عَنِ التَّكَلُّفِ».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 7293]
المزيــد ...

Imepokewa kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe ju yake- amesema:
Tulikuwa kwa Omari akasema: "Tumekatazwa kujilazimisha".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [Swahiih Al Bukhaariy - 7293]

Ufafanuzi

Anaeleza Omari -Radhi za Allaha ziwe juu yake- kwamba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- aliwakataza kuyafanya mambo yenye uzito bila kuwa na haja nayo, sawa sawa iwe ni kauli au kitendo.

Katika Faida za Hadithi

  1. Miongoni mwa kujikalifisha kuliko katazwa: Kuuliza uliza, au mtu kujikalifisha mambo asiyo na elimu nayo, au akalikazia jambo ambalo Mwenyezi Mungu kalipa nafasi pana.
  2. Ni lazima muislamu ailazimishe nafsi yake wepesi na kutojikalifisha katika kauli na vitendo: Katika kula kwake, na kunywa kwake, na maneno yake, na hali zake zote.
  3. Uislamu ni dini ya wepesi.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (62)