عن أبي الهياج الأسدي قال: قال لي علي رضي الله عنه : «ألا أَبْعَثُك على ما بَعَثَني عليه رسول الله صلى الله عليه وسلم ؟ أن لا تَدْعَ صُورَةً إلا طَمَسْتَها، ولا قَبْرًا مُشْرِفًا إلا سَوَّيْتَه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abii Hayyaji Al-Asadiy Amesema: Alisema kuniambia mimi Ally -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: "Je nikuagize katika yale aliyoniagiza kwayo Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake? Usiache picha yoyote ispokuwa umeifuta, wala kaburi lililonyanyuliwa ispokuwa umelisawazisha".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Uislamu unachunga sana juu ya kuziba kila mlango unaopelekea katika ushirikina uliofichikana au wa wazi, na ametueleza Ally- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: kuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake alimuagiza na akamuamrisha kuwa afute kila picha atakayoipata; jambo ambalo linaweza kumpelekea mfanyaji wake kuabudu masanamu. Na abomoe kila jengo lililojengwa juu ya kaburi au lililonyanyuliwa zaidi ya kiwango cha kisheria; kwa vile inavyokuwa katika kuyanyanyua miongoni mwa kufitinika wafanyaji wake, na kuwafanya waliyoko kaburini kuwa ni washirika wa Mwenyezi Mungu katika ibada na kuwatukuza. Na linafanyika hilo ili waislamu wabaki na uislamu wao, na ziwe safi itikadi zao; kwasababu kupiga picha na kuyajengea makaburi kunapelekea kuyakuza na kuyatukuza na kuyanyanyua zaidi ya nafasi yake, na kuyapa haki miongoni mwa haki za Mwenyezi Mungu Mtukufu.