عن أبي الهياج الأسدي قال: قال لي علي رضي الله عنه : «ألا أَبْعَثُك على ما بَعَثَني عليه رسول الله صلى الله عليه وسلم ؟ أن لا تَدْعَ صُورَةً إلا طَمَسْتَها، ولا قَبْرًا مُشْرِفًا إلا سَوَّيْتَه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Hayyaji Al-Asadiy Amesema: Alisema kuniambia mimi Ally -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: "Je nikuagize katika yale aliyoniagiza kwayo Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake? Usiache picha yoyote ispokuwa umeifuta, wala kaburi lililonyanyuliwa ispokuwa umelisawazisha".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Uislamu unachunga sana juu ya kuziba kila mlango unaopelekea katika ushirikina uliofichikana au wa wazi, na ametueleza Ally- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: kuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake alimuagiza na akamuamrisha kuwa afute kila picha atakayoipata; jambo ambalo linaweza kumpelekea mfanyaji wake kuabudu masanamu. Na abomoe kila jengo lililojengwa juu ya kaburi au lililonyanyuliwa zaidi ya kiwango cha kisheria; kwa vile inavyokuwa katika kuyanyanyua miongoni mwa kufitinika wafanyaji wake, na kuwafanya waliyoko kaburini kuwa ni washirika wa Mwenyezi Mungu katika ibada na kuwatukuza. Na linafanyika hilo ili waislamu wabaki na uislamu wao, na ziwe safi itikadi zao; kwasababu kupiga picha na kuyajengea makaburi kunapelekea kuyakuza na kuyatukuza na kuyanyanyua zaidi ya nafasi yake, na kuyapa haki miongoni mwa haki za Mwenyezi Mungu Mtukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Uharamu wa kupiga picha na ulazima wa kuziondoa picha na kuzifuta kwa aina zake zote.
  2. Kuusiana katika haki na kuamrisha mema na kukataza mabaya na kuifikisha elimu.
  3. Uharamu wa kuyanyanyua makaburi kwa kuyajengea au kwa linginelo; kwasababu jambo hilo ni katika njia za shirki.
  4. Ulazima wa kubomoa vijumba vilivyojengwa juu ya makaburi.
  5. Hakika kupiga picha ni kama kujengea juu ya makaburi, yote ni njia ya kuingia katika shirki.
  6. Inaingia katika kunyanyua ziada ya hayo ile michoro mikubwa inayokuwa juu makaburi, au michoro iliyotiwa rangi na ikapambwa, na watu huiita (mafungu).
Ziada