عن خولة بنت حكيم رضي الله عنها مرفوعًا: «مَن نزَل مَنْزِلًا فقال: أعوذ بكلمات الله التَّامَّات من شرِّ ما خلَق، لم يَضُرَّه شيءٌ حتى يَرْحَلَ مِن مَنْزِله ذلك».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Khaula binti Hakim- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakayeshuka mahala popote kisha akasema: -A'udhu bikalimaati llaahit taammaati min sharri maa khalaqa- (Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyotimia, kutokana na shari ya vile alivyoviumba), hakitomdhuru chochote mpaka aondoke mahala pake hapo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anauelekeza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Umma wake katika uombaji kinga wenye manufaa ambao unazuia kila lenye kuogopwa analoliogopa mwanadamu pale anaposhuka mahala katika ardhi, sawa sawa iwe safari au matembezi au kinginecho: kuwa ajikinge kwa maneno ya Mwenyezi Mungu Mwenye kutosheleza mwenye kukidhi aliyesalimika na kila aibu na mapungufu; Ili apate amani mahala pake hapo madamu bado yuko hapo, kwa kila lenye kuudhi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuomba kinga ni ibada.
  2. kuomba kinga kisheria ni kule kunakokuwa kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu au kwa majina ya mwenyezi Mungu na sifa zake.
  3. Nikuwa maneno ya Mwenyezi Mungu hayakuumbwa; kwasababu Mwenyezi Mungu ameweka sheria ya kuomba kinga kupitia hayo, na kuomba kinga kwa kiumbe ni shirki, ikajulisha kuwa hayakuumbwa.
  4. Ubora wa dua hii pamoja na ufupi wake.
  5. Nikuwa viumbe wote wapochini ya allah.
  6. Kubainishwa baraka za dua hii.
  7. Kubainishwa kuenea kwa Qur'ani na ukamilifu.