عن خولة بنت حكيم رضي الله عنها مرفوعًا: «مَن نزَل مَنْزِلًا فقال: أعوذ بكلمات الله التَّامَّات من شرِّ ما خلَق، لم يَضُرَّه شيءٌ حتى يَرْحَلَ مِن مَنْزِله ذلك».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Khaula binti Hakim- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakayeshuka mahala popote kisha akasema: -A'udhu bikalimaati llaahit taammaati min sharri maa khalaqa- (Najilinda kwa maneno ya Mwenyezi Mungu yaliyotimia, kutokana na shari ya vile alivyoviumba), hakitomdhuru chochote mpaka aondoke mahala pake hapo".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Anauelekeza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Umma wake katika uombaji kinga wenye manufaa ambao unazuia kila lenye kuogopwa analoliogopa mwanadamu pale anaposhuka mahala katika ardhi, sawa sawa iwe safari au matembezi au kinginecho: kuwa ajikinge kwa maneno ya Mwenyezi Mungu Mwenye kutosheleza mwenye kukidhi aliyesalimika na kila aibu na mapungufu; Ili apate amani mahala pake hapo madamu bado yuko hapo, kwa kila lenye kuudhi.