عن عوف بن مالك الأشجعي رضي الله عنه قال: كنا عند رسول الله صلى الله عليه وسلم تسعة أو ثمانية أو سبعة، فقال: «ألا تُبايعون رسول الله صلى الله عليه وسلم ؟» وكنَّا حَدِيث عهد بِبَيْعة، فقلنا: قد بايَعْنَاك يا رسول الله، ثم قال: «ألا تُبايعون رسول الله» فبَسَطْنَا أيْدِينا، وقلنا: قد بَايَعْناك فَعَلَام نُبايِعُك؟ قال: «على أن تعبدوا الله ولا تشركوا به شيئًا، والصلوات الخمس وتطيعوا الله» وأَسَر كلمة خفيفة «ولا تسألوا الناس شيئًا» فلقد رأيت بعض أولئك النَّفرَ يسقط سَوطُ أحدهم فما يسأل أحدًا يناولُه إيَّاه.
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aufu bin Maliki Al Ashjaiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Tulikuwa kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- watu tisa au nane au saba, akasema: "Hivi hamumpi ahadi ya utiifu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake-?" Na tulikuwa bado wageni tangu tulivyompa utiifu, tukasema: Hakika tumekupa utiifu ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, kisha akasema: "Hivi hamumpi ahadi ya utiifu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu " tukanyoosha mikono yetu, na tukasema: tayari tumekupa utiifu wetu ni kwa lipi tukupe utiifu? Akasema: "Juu ya kuwa mumuabudu Mwenyezi Mungu na wala msimshirikishe na chochote, na swala tano na mumtii Mwenyezi Mungu" Na akalificha neno hafifu (akazungumza kwa sauti ya chini) "Na wala msiwaombe watu chochote" hakika niliwaona baadhi ya watu wale unadondoka mjeredi wa mmoja wao na wala hamuombi yeyote amuokotee.
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Kutoka kwa Aufu bin Maliki Al Ashjaiy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: (Tulikuwa tumekaa kwa Mjumbe wa Mwenyezi Mungu akasema: Hivi hamumpi ahadi ya utiifu mjumbe wa Mwenyezi Mungu? na sisi tulikuwa hatuna muda mrefu tangu tulipotoa ahadi ya utiifu) ilikuwa ahadi hii ni usiku wa kuamkia baiatul 'aqaba (siku waliompa ahadi ya utiifu) kabla ya ahadi ya kuhama na ahadi ya jihadi na kuvumilia juu yake. Tukasema: (Tayari tushakupa ahadi ya utiifu ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu). Kisha akasema: "Hivi hamumpi ahadi ya utiifu Mjumbe wa Mwenyezi Mungu" akazidisha Abuudaudi katika riwaya yake baada ya kauli yao: tayari tushakupa ahadi ya utiifu, mpaka akayasema hayo mara tatu. kauli yake: (Tukanyoosha mikono yetu) yaani tukaitawanya kwa kumpa utiifu. Na tukasema: (tayari tumekupa utiifu ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu) Yaani: mara ya kwanza (ni kwa lipi jingine tukupe utiifu?) yaani ni kwa lipi tukupe utiifu wakati huu?. Akasema: (Mumuabudu) Yaani ninakupeni utiifu juu ya ibada ya Mwenyezi Mungu (peke yake) akiwa kapwekeka na katika hali ya utukufu (Na wala msimshirikishe na chochote) yaani katika ushirikina au vyenye kuabudiwa. (Na swala tano) yaani na mswali swala, kama alivyoweka wazi Abuudaudi. (Na mumtii Mwenyezi Mungu) yaani katika yote aliyokuamrisheni na kuyaepuka yale aliyokukatazeni. (Na akalifanya siri neno jepesi) alilifanya siri neno hili tofauti na yale yaliyokuwa kabla yake kwasababu yaliyokuwa kabla yake ni usia wa kiujumla, na sentensi hii inawahusu baadhi yao, na makusudio ya neno katika maana ya lugha ya kiarabu ni sentensi iliyotengenezwa, kwa kauli yake: (Na wala msiwaombe watu chochote) Amesema Al qurtubiy: Hili limechukuliwa katika tabia njema na kupata thamani ya kutokubeba neema za viumbe na kuitukuza subra, pamoja na maumivu ya shida na haja, na kutosheka na kutowahitajia watu, na kuitukuza nafsi. Amesema Aufu: (Hakika niliwaona baadhi ya watu katika kundi lile, unadondoka mjeredi wa mmoja wao wala hamuombi yeyote ampatie) Na makusudio yake: ni kuwaomba watu mali zao, wakaichukulia kiujumla wake, na kunakutakasa kile kichoitwa ombi hata kama ni dogo. Na huu ni ubainifu juu ya yale waliyokuwa nayo wema waliotangulia katika kuvifuatisha vitendo baada ya kauli, na kuifanyia kwao kazi elimu ambayo wameichukua kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na amepokea Imamu Ahmadi kutoka kwa Abuu Dhari: "Usimuombe yeyote chochote, hata kama utadondoka mjeredi wako na wala usichukue amana".

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama
Ziada