عن أبي موسى الأشعري رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «مثل الذي يذكر ربه والذي لا يذكره مثل الحي والميت» وفي رواية: «مثل البيت الذي يُذْكَرُ الله فيه، والبيت الذي لا يُذْكَرُ الله فيه، مثل الحيِّ والميِّت».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Musa Al Ash'ariy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Mfano wa yule anayemtaja Mola wake na yule asiyemtaja Mola wake ni mfano wa aliyehai na aliyekufa" Na katika riwaya nyingine: "Mfano wa nyumba anayotajwa Mwenyezi Mungu ndani yake, na nyumba asiyotajwa Mwenyezi Mungu ndani yake, ni mfano wa aliyehai na aliyekufa".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Maana ya hadithi: nikuwa anayemtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu basi Mwenyezi Mungu kauhuisha moyo wake kwa kumtaja yeye na akamfungua kifua chake, akawa ni kama aliyehai kwasababu ya kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu na kudumu juu ya hilo, kinyume na asiyemtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu, yeye ni kama maiti ambayo haina uhai. Yuko hai kwa mwili wake maiti kwa moyo wake. Na huu ni mfano ambao ni wajibu kwa mwanadamu kuuzingatia na ajue kuwa yeye kila anapoghafilika kumtaja Mwenyezi Mungu Mtukufu, basi moyo wake unapata ususuavu na huenda ukafa moyo wake, Mwenyezi Mungu atukinge na hilo. Amesema Mwenyezi Mungu Mtukufu: "Hivi aliyekuwa maiti tukamuhuisha na tukamjaalia nuru anayotembea nayo kwa watu, anaweza kuwa sawa mfano wake na aliyeko gizani si mwenye kutoka humo).

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama