عن طارق بن أشيم الأشجعي مرفوعاً: "من قال لا إله إلا الله، وكَفَرَ بما يُعْبَدُ من دون الله حَرُمَ مالُه ودمُه وحِسابُه على الله".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Twariq bin Ashiim A-Ashjaiy, Hadithi Marfu'u: "Atakayesema: Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, na akayapinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu, ni haramu mali yake, na damu yake, na hesabu yake ni juu ya Mwenyezi Mungu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anabainisha- Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii kuwa siyo haramu kuuwa mtu na kuchukua mali yake ispokuwa kwa ujumla wa mambo mawili: La kwanza: ni kauli ya Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu -Mtukufu-: La pili: Ni kupinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu -Mtukufu-, yakipatikana mambo haya mawili ni wajibu kumuacha kwa dhahiri na kukabidhi ndani yake kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu-, madamu hajaleta yanayohalalisha damu yake kama kuritadi au mali yake kama kuzuia zaka au heshima yake kama kuleta usumbufu katika kulipa deni.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa maana ya: Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu ni kuyapinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu katika masanamu na makaburi na mengineyo.
  2. Nikuwa kutamka Laa ilaaha illa llaah- Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu- ili mradi na kutopinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu hilo haliharamishi damu na mali hata kama atajua maana yake na akalifanyia kazi, anapokuwa hajaongeza katika hilo kuyapinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu.
  3. Nikuwa atakayeifanyia kazi tauhidi na akashikamana na sheria zake kwa muonekano ni wajibu kumuacha mpaka yadhihirike kwake yanayokwenda kinyume na hilo.
  4. Uwajibu wa kumuacha kafiri atakapoingia katika uislamu, hata kama ni katika hali ya mapigano mpaka ijulikane kwake kinyume na hivyo.
  5. Nikuwa mtu anaweza kusema: Laa ilaaha illa llaah- hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, wala hayapingi yanayoabudiwa kinyume na yeye.
  6. Nikuwa hukumu katika dunia ni katika dhahiri (yaani kile anachokidhihirisha mtu), na ama Akhera ni katika nia na makusudio.
  7. Uharamu wa damu ya muislamu na mali yake ispokuwa kwa haki.
  8. Ubora wa uislamu kiasi ambacho inalindwa damu ya mwenye kuukubali na mali yake.
  9. Uharamu wa kuchukua mali ya muislamu ispokuwa ile ya wajibu katika asili ya sheria kama zaka, au kumlipisha alichokiharibu.
Ziada