عن طارق بن أشيم الأشجعي مرفوعاً: "من قال لا إله إلا الله، وكَفَرَ بما يُعْبَدُ من دون الله حَرُمَ مالُه ودمُه وحِسابُه على الله".
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Twariq bin Ashiim A-Ashjaiy, Hadithi Marfu'u: "Atakayesema: Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, na akayapinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu, ni haramu mali yake, na damu yake, na hesabu yake ni juu ya Mwenyezi Mungu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Anabainisha- Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii kuwa siyo haramu kuuwa mtu na kuchukua mali yake ispokuwa kwa ujumla wa mambo mawili: La kwanza: ni kauli ya Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu -Mtukufu-: La pili: Ni kupinga yanayoabudiwa kinyume na Mwenyezi Mungu -Mtukufu-, yakipatikana mambo haya mawili ni wajibu kumuacha kwa dhahiri na kukabidhi ndani yake kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu-, madamu hajaleta yanayohalalisha damu yake kama kuritadi au mali yake kama kuzuia zaka au heshima yake kama kuleta usumbufu katika kulipa deni.