عَنِ ابْنِ عَبَّاسٍ رضي الله عنهما:
أَنَّ رَجُلًا أَتَى النَّبِيَّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ، فَكَلَّمَهُ فِي بَعْضِ الْأَمْرِ، فَقَالَ: مَا شَاءَ اللهُ وَشِئْتَ، فَقَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «أَجَعَلْتَنِي لِلَّهِ عَدْلًا؟ قُلْ: مَا شَاءَ اللهُ وَحْدَهُ».

[إسناده حسن] - [رواه ابن ماجه والنسائي في الكبرى وأحمد]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Bin Abbas -Radhi za Allah ziwe juu yao yeye na baba yake-:
Yakwamba mtu mmoja alikuja kwa Mtume rehema na amani zimfikie, akamsemesha katika baadhi ya mambo, akasema: Akitaka Mwenyezi Mungu na ukataka, akasema Mtume rehema na amani zimfikie: "Umenifanya mimi kuwa mshirika wa Mwenyezi Mungu? sema: Akitaka Mwenyezi Mungu pekee".

Upokezi wake ni mzuri - Imepokelewa na Ahmad

Ufafanuzi

Alikuja mtu mmoja kwa Mtume rehema na amani zimfikie akamsemesha kuhusu jambo lake binafsi, kisha akasema: "Akitaka Mwenyezi Mungu na ukataka wewe", Mtume rehema na amani zimfikie akaikemea kauli hii, na akamueleza kuwa kuunganisha matashi ya kiumbe na matashi ya Mwenyezi Mungu kwa kiunganishi "na" ni shirki ndogo, haifai kwa muislamu kuitamka, kisha akamuelekeza katika kauli ya sawa na ya haki: "Akitaka Mwenyezi Mungu peke yake", ampwekeshe Mwenyezi Mungu katika matashi, na wala asiunganishe matashi ya yeyote kwa aina yoyote ya kiunganishi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Katazo la kusema: Akitaka Mwenyezi Mungu na ukitaka, na mfano wake katika yale yanayounganisha matashi ya mja katika matashi ya Mwenyezi Mungu kwa "na"; kwani hii ni katika shirki ndogo.
  2. Ulazima wa kukemea uovu.
  3. Mtume rehema na amani zimfikie alilinda mipaka ya tauhidi, na akaziba njia za ushirikina.
  4. Wakati wa kuondoa uovu ni vyema kumuelekeza anayefikishiwa ujumbe katika mbadala wa halali, kwa kumuiga Mtume rehema na amani zimfikie.
  5. Kukusanya baina ya kauli yake rehema na amani zimfikie katika hadithi hii: "Akitaka Mwenyezi Mungu peke yake", na kauli yake katika hadithi nyingine: "Sema: Akitaka Mwenyezi Mungu kisha ukitaka wewe" Nikuwa kauli ya mtu: " Akitaka Mwenyezi Mungu kisha ukitaka wewe", hii inafaa, lakini kauli ya: "Akitaka Mwenyezi Mungu peke yake" ndio bora zaidi.
  6. Inafaa kusema: "Akitaka Mwenyezi Mungu kisha ukitaka" lakini bora zaidi ni kusema: "Akitaka Mwenyezi Mungu pekee".
Ziada