عن عبد الله بن عباس رضي الله عنهما قال: كنت خلف النبي صلى الله عليه وسلم يوماً فقال يا غلام، إني أعلمك كلمات: «احْفَظِ اللهَ يحفظْك، احفظ الله تَجِدْه تُجَاهَك، إذا سألت فاسأل الله، وإذا اسْتَعَنْتَ فاسْتَعِن بالله، واعلمْ أن الأمةَ لو اجتمعت على أن ينفعوك بشيء لم ينفعوك إلا بشيء قد كتبه الله لك، وإن اجتمعوا على أن يَضرُّوك بشيء لم يَضرُّوك إلا بشيء قد كتبه الله عليك، رفعت الأقلام وجفت الصحف».
وفي رواية: «احفظ الله تَجِدْه أمامك، تَعرَّفْ إلى الله في الرَّخَاء يَعرِفْكَ في الشِّدة، واعلم أنَّ ما أخطأَكَ لم يَكُنْ ليُصِيبَكَ، وما أصَابَكَ لم يَكُنْ لِيُخْطِئَكَ، واعلم أن النصرَ مع الصبرِ، وأن الفرجَ مع الكَرْبِ، وأن مع العُسْرِ يُسْرًا».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد بروايتيه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillah bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: "Nilikuwa nyuma ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake siku moja Akasema: Ewe kijana, hakika mimi ninakufundisha maneno: "Muhifadhi Mwenyezi Mungu atakuhifadhi, muhifadhi Mwenyezi Mungu utamkuta uendako, utakapoomba basi muombe Mwenyezi Mungu, na utakapotaka msaada basi taka msaada kwa Mwenyezi Mungu, na tambua yakuwa umma lau ungelikusanyika juu ya kukunufaisha wewe wasingelikunufaisha ila kwa kitu alichokiandika Mwenyezi Mungu kuwa kikunufaishe, na kama watakusanyika juu ya kukudhuru wewe kwa kitu chochote, hawatoweza kukudhuru ila kwa kitu alichokiandika Mwenyezi Mungu kuwa kitakudhuru, kalamu zimenyanyuliwa, na kurasa zimekauka". Na katika riwaya nyingine: "Muhifadhi Mwenyezi Mungu utamkuta mbele yako, jipendekeze kwa Mwenyezi Mungu wakati wa raha atakujua wakati wa shida, najua kuwa yaliyokukosa hayakuwa ni yenye kukupata, na yaliyokupata hayakuwa ni yenye kukukosa, najua kuwa msaada (nusra) huendana pamoja na subira, nakuwa faraja huendana pamoja na matatizo, na hakika palipo na uzito pana wepesi".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy
Katika hadithi hii tukufu anamuelekeza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kijana huyu ambaye ni Ibn Abbasi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- usia mtukufu unaoambatana nakuwa ahifadhi amri za Mwenyezi Mungu Mtukufu na makatazo yake katika nafasi zake zote na nyakati zake zote, na anamsahihisha Mtume itikadi utotoni kuwa hakuna muumbaji ispokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna awezae ispokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna mpangiliaji wa mambo pamoja na Mwenyezi Mungu, na hakuna muwakilishi kati ya mja na Mola wake na msimamizi wake katika kutegemea na kuomba, ni yeye aliyetakasika mwenye kutarajiwa wakati wa kushuka matatizo, na yeye aliyetakasika ndiye mwenye kutarajiwa zinapotokea adhabu, na akapanda Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake katika nafsi ya Ibn Abbas- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kuamini makadirio ya Mwenyezi Mungu na hukumu yake, kila kitu ni kwa kadari yake Mtukufu na hukumu yake, miongoni mwa kheri au shari, nakuwa watu wote hawamiliki mikononi mwao kutimiza yote wanayoyataka, na hayawi ila aliyoyaidhinisha Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka.