عن عبد الله بن عباس رضي الله عنهما قال: كنت خلف النبي صلى الله عليه وسلم يوماً فقال يا غلام، إني أعلمك كلمات: «احْفَظِ اللهَ يحفظْك، احفظ الله تَجِدْه تُجَاهَك، إذا سألت فاسأل الله، وإذا اسْتَعَنْتَ فاسْتَعِن بالله، واعلمْ أن الأمةَ لو اجتمعت على أن ينفعوك بشيء لم ينفعوك إلا بشيء قد كتبه الله لك، وإن اجتمعوا على أن يَضرُّوك بشيء لم يَضرُّوك إلا بشيء قد كتبه الله عليك، رفعت الأقلام وجفت الصحف». وفي رواية: «احفظ الله تَجِدْه أمامك، تَعرَّفْ إلى الله في الرَّخَاء يَعرِفْكَ في الشِّدة، واعلم أنَّ ما أخطأَكَ لم يَكُنْ ليُصِيبَكَ، وما أصَابَكَ لم يَكُنْ لِيُخْطِئَكَ، واعلم أن النصرَ مع الصبرِ، وأن الفرجَ مع الكَرْبِ، وأن مع العُسْرِ يُسْرًا».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد بروايتيه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abdillah bin Abbas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Amesema: "Nilikuwa nyuma ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake siku moja Akasema: Ewe kijana, hakika mimi ninakufundisha maneno: "Muhifadhi Mwenyezi Mungu atakuhifadhi, muhifadhi Mwenyezi Mungu utamkuta uendako, utakapoomba basi muombe Mwenyezi Mungu, na utakapotaka msaada basi taka msaada kwa Mwenyezi Mungu, na tambua yakuwa umma lau ungelikusanyika juu ya kukunufaisha wewe wasingelikunufaisha ila kwa kitu alichokiandika Mwenyezi Mungu kuwa kikunufaishe, na kama watakusanyika juu ya kukudhuru wewe kwa kitu chochote, hawatoweza kukudhuru ila kwa kitu alichokiandika Mwenyezi Mungu kuwa kitakudhuru, kalamu zimenyanyuliwa, na kurasa zimekauka". Na katika riwaya nyingine: "Muhifadhi Mwenyezi Mungu utamkuta mbele yako, jipendekeze kwa Mwenyezi Mungu wakati wa raha atakujua wakati wa shida, najua kuwa yaliyokukosa hayakuwa ni yenye kukupata, na yaliyokupata hayakuwa ni yenye kukukosa, najua kuwa msaada (nusra) huendana pamoja na subira, nakuwa faraja huendana pamoja na matatizo, na hakika palipo na uzito pana wepesi".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Katika hadithi hii tukufu anamuelekeza Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kijana huyu ambaye ni Ibn Abbasi Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- usia mtukufu unaoambatana nakuwa ahifadhi amri za Mwenyezi Mungu Mtukufu na makatazo yake katika nafasi zake zote na nyakati zake zote, na anamsahihisha Mtume itikadi utotoni kuwa hakuna muumbaji ispokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna awezae ispokuwa Mwenyezi Mungu, na hakuna mpangiliaji wa mambo pamoja na Mwenyezi Mungu, na hakuna muwakilishi kati ya mja na Mola wake na msimamizi wake katika kutegemea na kuomba, ni yeye aliyetakasika mwenye kutarajiwa wakati wa kushuka matatizo, na yeye aliyetakasika ndiye mwenye kutarajiwa zinapotokea adhabu, na akapanda Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake katika nafsi ya Ibn Abbas- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- kuamini makadirio ya Mwenyezi Mungu na hukumu yake, kila kitu ni kwa kadari yake Mtukufu na hukumu yake, miongoni mwa kheri au shari, nakuwa watu wote hawamiliki mikononi mwao kutimiza yote wanayoyataka, na hayawi ila aliyoyaidhinisha Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kufaa kupakizana juu ya mnyama ikiwa ataweza.
  2. Ameeleza mwalimu kwa mwanafunzi kuwa yeye anataka kumfundisha kabla ya kufanya hivyo, ili iongezeke shauku yake katika yale anayofundishwa na nafsi yake iyakubali.
  3. Kumhurumia Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake aliye chini yake, pale aliposema: "Ewe kijana hakika mimi ninakufundisha maneno".
  4. Ubora wa Ibn Abbas- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-, kiasi ambacho Mtume alimuona kuwa anastahiki kupewa usia huu pamoja na udogo wa umri wake.
  5. Malipo yanaweza kuwa kulingana na matendo.
  6. Amri ya kutegemea kwa Mwenyezi Mungu, na kumtegemea yeye bila mwingine asiyekuwa yeye, na yeye ndiye mtetezi bora.
  7. Kushindwa kwa viumbe wote, na kuhitaji kwao kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  8. Tahadhari juu ya nyumba hii (Dunia) kuwa ni sehemu ya mitihani, hivyo ni lazima kuvumilia juu yake.
  9. Kuridhika na hukumu na mipangilio.
  10. Atakayempoteza Mwenyezi Mungu -yaani akaipoteza dini yake- basi Mwenyezi Mungu atampoteza na wala hatomuhifadhi.
  11. Atakayemuhifadhi Mwenyezi Mungu Mtukufu atamuongoza na atamuelekeza katika yale yenye kheri.
  12. Habari njema kubwa kwa mwanadamu kuwa pale unapompata uzito basi asubiri wepesi.
  13. Kuliwazwa mja pale inapotokea mitihani, na kuyakosa yale ayapendayo, kwa mujibu wa moja kati ya maana mbili katika kauli yake: "Na tambua kuwa yaliyokufika hayakuwa ni yenye kukukosa, na yaliyokukosa hayakuwa ni yenye kukupata" Sentensi ya kwanza ni kuliwazwa wakati wa kufikwa na yenye kuchukiza, na ya pili ni katika kuyakosa yale yenye kupendeka.