عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: «لَعَن رسول الله صلى الله عليه وسلم الرَّاشِي والمُرْتَشِي في الحُكْم».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: "Amemlaani Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake- mtoa rushwa na mpokea rushwa katika hukumu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Kwakuwa rushwa ni kutoa mali ili iwe ni sababu ya kuifikia batili, ameomba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kufukuzwa na kuwekwa mbali na rehma za Mwenyezi Mungu kwa mtoaji wake na mpokeaji wake; kwasababu ya yale yaliyomo miongoni mwa madhara kwa mtu mmoja mmoja na jamii nzima, na rushwa imeharamishwa moja kwa moja, na imekuja rasmi hukumu katika hadithi; kwasababu rushwa kwaajili hukumu ni jambo kubwa kwa kile kilichomo miongoni mwa kubadili hukumu ya sheria, kwa kumpa hakimu kitu ambacho kitaleta athari ya kubadili hukumu au kuipunguza na kuifanya kuwa inafaa kwa yule aliyetoa rushwa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ni haramu kutoa rushwa, na kuichukua, na kuwa wakala wake, na kusaidia kuifanikisha, kwa kile kilichomo katika kusaidizana juu ya batili.
  2. Rushwa ni katika madhambi makubwa; kwasababu Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amemlaani mpokeaji wake na mtoaji wake, na laana haiwi ila kwa dhambi kubwa miongoni mwa madhambi makubwa, na wamekubaliana wanachuoni juu ya kuiharamisha kwake.
  3. Rushwa katika mlango wa maamuzi na hukumu ni kosa kubwa, na ni dhambi mbaya, miongoni mwa kile kilichomo katika kula mali za watu kwa batili na kubadili hukumu ya Mwenyezi Mungu Mtukufu-, na kuhumu kinyume na yale aliyoyateremsha Mwenyezi Mungu; na mpokeaji wake ameidhulumu nafsi yake kwa kuipokea kwake, na amedhulumu kile kinachohukumiwa, na kamdhulumu yule anayehukumiwa.
Ziada