عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: «لَعَن رسول الله صلى الله عليه وسلم الرَّاشِي والمُرْتَشِي في الحُكْم».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: "Amemlaani Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake- mtoa rushwa na mpokea rushwa katika hukumu".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy
Kwakuwa rushwa ni kutoa mali ili iwe ni sababu ya kuifikia batili, ameomba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake kufukuzwa na kuwekwa mbali na rehma za Mwenyezi Mungu kwa mtoaji wake na mpokeaji wake; kwasababu ya yale yaliyomo miongoni mwa madhara kwa mtu mmoja mmoja na jamii nzima, na rushwa imeharamishwa moja kwa moja, na imekuja rasmi hukumu katika hadithi; kwasababu rushwa kwaajili hukumu ni jambo kubwa kwa kile kilichomo miongoni mwa kubadili hukumu ya sheria, kwa kumpa hakimu kitu ambacho kitaleta athari ya kubadili hukumu au kuipunguza na kuifanya kuwa inafaa kwa yule aliyetoa rushwa.