+ -

عن أبي هريرة رضي الله عنه قال:
لَعَنَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ الرَّاشِيَ وَالْمُرْتَشِيَ فِي الْحُكْمِ.

[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد] - [سنن الترمذي: 1336]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Allah ziwe juu yake alisema:
"Amemlaani Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake- mtoa rushwa na mpokea rushwa katika hukumu".

Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Aliomba Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kufukuzwa na kuwekwa mbali na rehema ya Mwenyezi Mungu Mtukufu mtoa rushwa na mchukuaji wake na mpokeaji wake.
Na miongoni mwake ni kile kinachotolewa kwa mahakimu ili wapindishe hukumu wanayoisimamia; ili mtoaji aitumie kama njia ya kufikia lengo lake pasina haki.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية القيرقيزية النيبالية اليوروبا الليتوانية الدرية الصومالية الكينياروندا التشيكية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ni haramu kutoa rushwa, na kuichukua, na kuwa wakala wake, na kusaidia; kwa sababu ndani yake kuna kusaidizana katika batili.
  2. Rushwa ni katika madhambi makubwa; kwa sababu Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kamlaani mpokeaji wake na mtoaji wake.
  3. Rushwa katika mlango wa kesi na hukumu ni dhulma kubwa na ni dhambi kubwa mno; kwani hapa kuna dhulma na kuhukumu kwa yale ambayo hakuyateremsha Mwenyezi Mungu.
Ziada