عن أنس رضي الله عنه : أن النبي صلى الله عليه وسلم ومعاذ رديفه على الرَّحْلِ، قال: «يا معاذ» قال: لبَّيْكَ يا رسول الله وسَعْدَيْكَ، قال: «يا معاذ» قال: لَبَّيْكَ يا رسول الله وسَعْدَيْكَ، قال: «يا معاذ» قال: لبَّيْكَ يا رسول اللهِ وسَعْدَيْكَ، ثلاثا، قال: «ما من عبد يشهد أن لا إله إلا الله، وأَنَّ محمدا عبده ورسوله صِدْقًا من قلبه إلَّا حرمه الله على النار» قال: يا رسول الله، أفلا أُخْبِر بها الناس فَيَسْتَبْشِرُوا؟ قال: «إِذًا يتكلوا» فأخبر بها معاذ عند موته تَأَثُّمًا.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- na Mua'dh akiwa nyuma yake juu ya kipandwa, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema hivyo mara tatu, Akasema: "Hakuna mja yeyote atakayeshuhudia kuwa Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake kiukweli toka moyoni mwake ispokuwa atamharamisha Mwenyezi Mungu kuingia motoni" Akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu hivi nisiwaeleze watu hili ili wajipe bishara (matumaini)? Akasema: "Basi watabweteka" Akalizungumza hilo Mua'dh wakati wa kifo chake kwa kuhofia kupata dhambi.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Alikuwa Mu'adh kapanda nyuma ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, Akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Ewe Mu'adh; Akasema: Naam -Nimekuitikia Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na furaha ni yako, yaani jibu moja baada ya jingine, na kwa kukutii wewe, nimefurahisha utiifu wako kwa kukufurahisha wewe baada ya furaha, kisha akasema: Ewe Mu'adh; Akasema: Naam -Nimekuitikia Ewe Mjumbe na furaha ni yako, kisha akasema: Ewe Mu'adh; Akasema: Naam -Nimekuitikia Ewe Mjumbe na furaha ni yako, "Hakuna mja yeyote atakayeshuhudia kuwa Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake kiukweli toka moyoni mwake hasemi tu kwa ulimi wake; Ispokuwa atamharamishia Mwenyezi Mungu kukaa milele motoni; Akasema Mu'adh: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu je niwaeleze watu ili niwaingizie furaha, Akasema Rehema na Amani ziwe juu yake: Hapana ili wasitegemee hilo na wakaacha kufanya matendo, akalieleza Mu'adh mwisho wa uhai wake kwa kuhofia madhambi ya kuficha elimu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuacha kusimulia hadithi itakapokuwa inaambatana na katazo, au kukaa na kuacha kufanya yaliyo bora kuliko hilo.
  2. Kufaa kupakizana juu ya mnyama kwa sharti la kutomdhuru.
  3. Kubainishwa nafasi ya Mu'adh kwa Mtume rehema na Amani ziwe juu yake na mapenzi yake kwake.
  4. Kufaa kutaka ufafanuzi katika yale yanayotatiza katika nafsi ya muulizaji.
  5. Katika sharti za kushuhudia kuwa hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu na Muhammadi ni Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, anatakiwa msemaji wake awe mkweli asiwe mwenye shaka wala mnafiki.
  6. Wenye kumpwekesha Mwenyezi Mungu hawatokaa milele katika moto wa Jahannam, hata kama watauingia kwasababu ya madhambi yao, watatolewa baada ya kusafishwa.