عن أنس رضي الله عنه : أن النبي صلى الله عليه وسلم ومعاذ رديفه على الرَّحْلِ، قال: «يا معاذ» قال: لبَّيْكَ يا رسول الله وسَعْدَيْكَ، قال: «يا معاذ» قال: لَبَّيْكَ يا رسول الله وسَعْدَيْكَ، قال: «يا معاذ» قال: لبَّيْكَ يا رسول اللهِ وسَعْدَيْكَ، ثلاثا، قال: «ما من عبد يشهد أن لا إله إلا الله، وأَنَّ محمدا عبده ورسوله صِدْقًا من قلبه إلَّا حرمه الله على النار» قال: يا رسول الله، أفلا أُخْبِر بها الناس فَيَسْتَبْشِرُوا؟ قال: «إِذًا يتكلوا» فأخبر بها معاذ عند موته تَأَثُّمًا.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-: Yakwamba Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- na Mua'dh akiwa nyuma yake juu ya kipandwa, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema: "Ewe Mua'dh" Akasema: Labaika Wasa'daika- Nimekuitikia kwa furaha yako- Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, Alisema hivyo mara tatu, Akasema: "Hakuna mja yeyote atakayeshuhudia kuwa Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake kiukweli toka moyoni mwake ispokuwa atamharamisha Mwenyezi Mungu kuingia motoni" Akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu hivi nisiwaeleze watu hili ili wajipe bishara (matumaini)? Akasema: "Basi watabweteka" Akalizungumza hilo Mua'dh wakati wa kifo chake kwa kuhofia kupata dhambi.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Alikuwa Mu'adh kapanda nyuma ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, Akasema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Ewe Mu'adh; Akasema: Naam -Nimekuitikia Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na furaha ni yako, yaani jibu moja baada ya jingine, na kwa kukutii wewe, nimefurahisha utiifu wako kwa kukufurahisha wewe baada ya furaha, kisha akasema: Ewe Mu'adh; Akasema: Naam -Nimekuitikia Ewe Mjumbe na furaha ni yako, kisha akasema: Ewe Mu'adh; Akasema: Naam -Nimekuitikia Ewe Mjumbe na furaha ni yako, "Hakuna mja yeyote atakayeshuhudia kuwa Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, nakuwa Muhammadi ni mja wake na ni Mtume wake kiukweli toka moyoni mwake hasemi tu kwa ulimi wake; Ispokuwa atamharamishia Mwenyezi Mungu kukaa milele motoni; Akasema Mu'adh: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu je niwaeleze watu ili niwaingizie furaha, Akasema Rehema na Amani ziwe juu yake: Hapana ili wasitegemee hilo na wakaacha kufanya matendo, akalieleza Mu'adh mwisho wa uhai wake kwa kuhofia madhambi ya kuficha elimu.