عَنْ عُمَرَ بْنِ الخَطَّابِ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ:
قَدِمَ عَلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ سَبْيٌ، فَإِذَا امْرَأَةٌ مِنَ السَّبْيِ قَدْ تَحْلُبُ ثَدْيَهَا تَسْقِي، إِذَا وَجَدَتْ صَبِيًّا فِي السَّبْيِ أَخَذَتْهُ، فَأَلْصَقَتْهُ بِبَطْنِهَا وَأَرْضَعَتْهُ، فَقَالَ لَنَا النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ: «أَتُرَوْنَ هَذِهِ طَارِحَةً وَلَدَهَا فِي النَّارِ؟» قُلْنَا: لاَ، وَهِيَ تَقْدِرُ عَلَى أَلَّا تَطْرَحَهُ، فَقَالَ: «لَلَّهُ أَرْحَمُ بِعِبَادِهِ مِنْ هَذِهِ بِوَلَدِهَا».
[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 5999]
المزيــد ...
Imepokewa Kutoka kwa Omar bin Khattwab -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema:
Walikuja mateka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, mara kukawa na mwanamke miongoni mwa mateka akikamua maziwa yake na kunyonyesha, akipata mtoto katika mateka anamchukua, anamkumbatia na kumuweka tumboni kwake na kumnyonyesha, basi Mtume rehema na amani ziwe juu yake akasema kutuambia: "Hivi mnadhani mwanamke huyu anaweza kumtupa mwanaye motoni?" Tukasema: Hapana, hawezi kumtupa, akasema: "Basi Mwenyezi Mungu ana huruma zaidi kwa waja wake kuliko mwanamke huyu kwa mtoto wake".
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 5999]
Waliletwa mateka kwa Mtume rehema na amani ziwe juu yake kutoka katika kabila la Hawazini, mara kukawa na mwanamke miongoni mwao akimtafuta mwanaye, kila akipata mtoto anamnyonyesha kwa sababu ya kudhurika kwake kwa wingi wa maziwa katika matiti yake, mara, akampata mwanaye katika mateka akamchukua, akamkumbatia tumboni kwake na akamnyonyesha, akasema Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwaambia Maswahaba zake: Hivi mnadhani mwanamke huyu anaweza kumtupa mwanaye motoni? Tukasema: Kamwe, hawezi kumtuka kwa hiyari yake milele. Akasema: Basi Mwenyezi Mungu ana huruma zaidi kwa waja wake Waislamu kuliko mwanamke huyu kwa mtoto wake.