عن أبي قتادة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «الرُّؤْيَا الصَّالِحَةُ -وفي رواية: الرُّؤْيَا الحَسَنَةُ- من الله، والحُلُمُ من الشيطان، فمن رأى شيئًا يَكْرَهُهُ فَلْيَنْفُثْ عن شماله ثلاثا، وَلْيَتَعَوَّذْ من الشيطان؛ فإنها لا تضره». وعن جابر رضي الله عنه عن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «إذا رأى أحدكم الرُّؤْيَا يَكْرَهُهَا، فَلْيَبْصُقْ عن يساره ثلاثا، ولْيَسْتَعِذْ بالله من الشيطان ثلاثا، ولْيَتَحَوَّلْ عن جَنْبِه الذي كان عليه».
[صحيح] - [حديث أبي قتادة: متفق عليه. حديث جابر: رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Qatada -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Ndoto njema -na katika riwaya nyingine: ndoto nzuri- hutoka kwa Mwenyezi Mungu, na njozi hutoka kwa shetani, atakayeota kitu anachokichukia basi ateme kushotoni kwake mara tatu, na aombe kinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani;kwani hilo haliwezi kumdhuru".Na kutoka kwa Jabiri -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakapoona mmoja wenu ndoto anayoichukia,basi ateme kushotoni kwake mara tatu, na aombe kinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani mara tatu, na ageuze ubavu tofauti na ule aliokuwa kalalia".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Ameeleza -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika hadithi hii:kuwa ndoto iliyosalimika inatokana na mvurugo wa shetani na ushawishi wake,hiyo ni miongoni mwa neema za Mwenyezi Mungu juu ya waja wake,na ni katika habari njema kwa waumini,na ni tahadhari kwa walioghafilika, na ni ukumbusho kwa wenye kupuuza.Na njoza ambazo ni ndoto zilizoparaganyika,hii ni mvurugo wa shetani juu ya roho ya mwanadamu, na ushawishi wake juu yake na kumhuzunisha,na ni kuleta mambo ambayo yatakayomsababishia misongo na huzuni na huenda akaugua; kwasababu shetani ni adui wa mwanadamu anapenda yanayomchukiza na yanayomuhuzunisha. Atakapoona mtu usingizini mwake yanayomkera na kumuogopesha na kumuhuzunisha,anatakiwa achukue sababu zinazozuia vitimbi vya shetani na wasiwasi wake,na tiba ni kama ilivyokuja katika hadithi:Kwanza: Ateme kushotoni kwake mara tatu.Pili: Ajikinge kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shetani aliyelaaniwa mara tatu kwaajili ya kuzuia shari yake na ubaya wake.Tatu:Atakapokuwa kalalia ubavu wa kushoto basi anajigeuza ubavu wa kulia, na kama ni ubavu wa kulia basi anageuzia wa kushoto. Atakapofanya sababu zilizotangulia hakuna chochote kitakachomdhuru kwa idhini ya Mwenyezi Mungu afanye hivyo kwa kusadikisha kauli ya Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake,na awe na uhakika wa kufanikiwa kwa sababu za kuzuia alizozifanya.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri
Kuonyesha Tarjama