عن أنس بن مالك رضي الله عنه مرفوعاً: «إن الله ليرضى عن العبد أن يأكل الأكلة، فيحمده عليها، أو يشرب الشَّربة، فيحمده عليها».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas bin Maliki Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Hakika Mwenyezi Mungu huridhika kwa mja anapokula chochote, akamshukuru juu ya hicho, au akanywa chochote akamshukuru juu ya hicho".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Hakika katika sababu za kumridhisha Mwenyezi Mungu Mtukufu ni kumshukuru juu ya kula na kunywa, kwani yeye Mtukufu peke yake, ndiye anayetoa fadhila kwa riziki hii.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuthibitisha sifa ya kuridhika kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu.
  2. Nikuwa radhi za Mwenyezi Mungu hupatikana kwa sababu ndogo sana kama kushukuru baada ya kula na kunywa.
  3. Kuhimizwa juu ya kumshukuru Mwenyezi Mungu Mtukufu, nakuwa hilo ni sababu ya kuridhika kwake, nakuwa shukurani ni njia ya kusalimika na kukubaliwa.
  4. Kubainishwa adabu katika adabu za vyakula na vinywaji.
  5. Kubainishwa ukarimu wa Mwenyezi Mungu Mtukufu, Hakika amekupendelea juu yako wewe kwa riziki na akaridhia kutoka kwako shukurani.
  6. Sunna -mafundisho- huwa kwa kusema: Al-hamdulillaah (kila sifa njema zinamstahiki Mwenyezi Mungu).