عَنْ عَائِشَةَ أُمِّ المُؤْمِنين رضي الله عنها زَوْجِ النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ أَنَّ رَسُولَ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«يَا عَائِشَةُ إِنَّ اللهَ رَفِيقٌ يُحِبُّ الرِّفْقَ، وَيُعْطِي عَلَى الرِّفْقِ مَا لَا يُعْطِي عَلَى الْعُنْفِ، وَمَا لَا يُعْطِي عَلَى مَا سِوَاهُ».
[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2593]
المزيــد ...
Kutoka kwa Aisha Mama wa Waumini radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake, mke wa Mtume rehema na amani ziwe juu yake, ya kwamba Mtume rehema na amani ziwe juu yake alisema:
"Ewe Aisha, hakika Mwenyezi Mungu ni Mpole anapenda upole, na hutoa malipo katika upole ambayo hayatoi katika ususuwavu (ukali), na wala hatoi kwa mengineyo".
[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 2593]
Alimuhimiza Mtume rehema na amani ziwe juu yake mama wa Waumini Aisha radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake juu ya upole, na kwamba Mwenyezi Mungu ni Mpole kwa waja wake anawatakia wepesi na wala hawatakii ugumu, wala hawalazimishi juu ya uwezo wao, ni wajibu kwa mja wake ajipambe kwa ulaini na kuchukua kilicho rahisi; asiwe mkorofi wala mkali, na kwamba Mwenyezi Mungu Mtukufu hutoa malipo kwa sababu ya upole na ulaini katika dunia kama kusifia vizuri, na kutoa mahitaji ya watu na kurahisisha malengo, na Akhera kutoa thawabu nyingi zaidi kuliko jinsi anavyotoa katika ususuwavu na ukali na ukorofi, upole huja na mambo ambayo hayaji katika mambo mengine.