+ -

عن عائشة رضي الله عنها زوج النبي صلى الله عليه وسلم عن النبي صلى الله عليه وسلم قال:
«إِنَّ الرِّفْقَ لَا يَكُونُ فِي شَيْءٍ إِلَّا زَانَهُ، وَلَا يُنْزَعُ مِنْ شَيْءٍ إِلَّا شَانَهُ».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 2594]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Allah ziwe kwake- mke wa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- anasimulia kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- alisema:
"Hakika upole hauwi ndani ya kitu isipokuwa hukipendezesha, na hautolewi ndani ya kitu ila hukichafua".

Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Anabainisha Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- yakuwa upole na ulaini na utaratibu katika kauli na matendo huyazidishia mambo uzuri na ukamilifu na ubora, na mtu mwenye sifa hizi hakika anastahiki kupata hitajio lake.
Na kukosekana kwa upole huyatia aibu mambo na kuyatia sura mbaya na humkwamisha mtu kupata shida yake, na hata akiipata huipata kwa tabu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية القيرقيزية النيبالية اليوروبا الليتوانية الدرية الصومالية الكينياروندا الرومانية المجرية التشيكية المالاجاشية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Himizo la kujipamba na upole.
  2. Upole humpamba mtu, nayo ni sababu ya kila heri katika mambo ya Akhera na Dunia.