+ -

عن حُذَيْفَةَ بْنِ الْيَمَانِ رضي الله عنهما مرفوعاً: «لا تلْبَسُوا الحرير ولا الديباج، ولا تشربوا في آنية الذهب والفضة ولا تأكلوا في صِحَافِهِمَا؛ فإنَّهَا لهم في الدنيا ولكم في الآخرة».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Imesimuliwa kutoka kwa Abdul-Rahman bin Abi Laila, kuwa, siku moja walikuwa kwa Hudhaifa, akaomba maji, Mmajusi mmoja akampa kitu cha kunywa, alipokiweka kikombe mkononi mwake, akakitupa, na akasema: Kwani si nilishamkataza zaidi ya mara moja au mbili - kana kwamba anasema: Sikufanya hivi kwa matashi yangu - bali nilimsikia Mtume, rehema na amani ziwe juu yake akisema:
“Msivae hariri wala dibaji (Sufi) wala msinywe katika vyombo vya dhahabu au vya fedha, wala msile katika vyombo vilivyotengenezwa kwa dhahabu na fedha, kwani ni vyao (Makafiri) katika dunia na sisi ni vyetu Akhera."

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Mtume, Rehema na Amani zimshukie, amekataza wanaume kuvaa hariri za kila aina. Aliwakataza wanaume na wanawake kula na kunywa katika vyombo vya dhahabu na fedha. Akasema kuwa ni kwa ajili ya waumini tu Siku ya Kiyama; Kwa sababu waliviepuka katika ulimwengu huu kwa kumtii Mwenyezi Mungu, Ama makafiri wao si vyao huko akhera. Kwa sababu waliharakisha vizuri vyao katika maisha yao ya dunia kwa kuvitumia, na kuasi kwao amri ya Mwenyezi Mungu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Thai Kiassam السويدية الأمهرية الغوجاراتية القيرقيزية اليوروبا الدرية الصومالية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Katazo kwa wanaume la kuvaa hariri na dibaji, na kuwatishia vikali wale wenye kuvaa.
  2. Inafaa kwa wanawake kuvaa hariri na nguo iliyotengenezwa kwa hariri
  3. Uharamu wa kula na kunywa katika sahani za dhahabu na fedha na vyombo vyake, kwa wanaume na wanawake.
  4. Hudhaifa, Mwenyezi Mungu amuwie radhi, alikuwa mkali katika kukemea kwake, na akaeleza hayo kwa kusema kwamba alimkataza zaidi ya mara moja kutumia vyombo vya dhahabu na fedha, lakini hakuacha.