عَنْ عُمَرَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ النَّبِيُّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«مَنْ لَبِسَ الحَرِيرَ فِي الدُّنْيَا لَمْ يَلْبَسْهُ فِي الآخِرَةِ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 5834]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Omari radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake:
"Atakayevaa hariri duniani hatoivaa Akhera"

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhari na Muslim juu ya usahihi wake] - [Swahiih Al Bukhaariy - 5834]

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa mwanaume yeyote atakayevaa hariri duniani hatovaa Akhera endapo hatotubia, na hii ni adhabu kwake.

Katika Faida za Hadithi

  1. Makusudio ya hariri ni hariri halisi ya asili, ama hariri ya bandia ya viwandani haihusiki hapa katika hadithi.
  2. Katazo la kuvaa hariri kwa wanaume.
  3. Katazo la kuvaa hariri linahusu kuivaa na kuitandika.
  4. Wanaume wanaruhusiwa kutumia hariri katika nguo ila isizidi kiwango cha vidole viwili mpaka vinne, itakayofanywa kama mchoro au urembo wa nguo.
Kuonyesha Tarjama
Lugha: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Ziada (51)