عن أبي هريرة رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «من رآني في المنام فَسَيَرَانِي في اليَقظة -أو كأنما رآني في الْيَقَظَةِ- لا يَتَمَثَّلُ الشيطان بي».
[صحيح] - [متفق عليه. مسلم]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake-: "Atakayeniona mimi ndotoni basi ataniona akiwa macho -au ni kana kwamba kaniona akiwa macho- hajifananishi shetani na mimi".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim

Ufafanuzi

Wametofautiana wanachuoni katika kubainisha maana ya hadithi hii, katika mitazamo mingi: Wa kwanza: Nikuwa makusudio yake: ni wale watu wa zama zake, na maana yake nikuwa atakayemuona usingizini na akawa hakuhama, hajawezeshwa na Mwenyezi Mungu Mtukufu kuhama na kumuona yeye -Rehema na Amani ziwe juu yake- akiwa macho wazi. Na ya pili: Nikuwa anayeonekana kwake usingizini ndiye Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- halisi, yaani katika ulimwengu wa roho, na kuwa kumuona kwake ni kweli, lakini sharti iwe kwa sifa yake inayojulikana-. Ya tatu: Nikuwa yeye ataona uhakika wa hiyo ndoto akiwa macho akhera; ni kumuona maalumu kwasababu ya kuwa karibu naye na kupata utetezi wake na mfano wa hayo. Kauli yake: "Au ni kana kwamba kaniona akiwa macho" Hii ni riwaya ya Imamu Muslim kaipokea ikiwa na shaka katika mapokezi yake: Je alisema -Rehema na Amani ziwe juu yake- "Ataniona akiwa macho?" au alisema: "Ni kana kwamba kaniona akiwa macho". Na maana yake: nikuwa atakayemuona Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika ndoto kwa sifa zake ambazo yeye yuko nazo basi ni kana kwamba kamuona akiwa macho, hii ni kama kauli yake -Rehema na Amani ziwe juu yake-, kama ilivyokuja katika sahihi mbili (yaani kitabu cha sahihi Bukhariy na sahihi Muslim): "Atakayeniona ndotoni, basi atakuwa kaniona" na katika riwaya nyingine ndani ya sahihi mbili pia: "Atakayeniona ndotoni, basi atakuwa kaniona mimi kweli". kauli yake: "Hajifananishi shetani na mimi", na katika tamko jingine: "Atakayeniota mimi usingizini atakuwa kaniona mimi, kwani hakika haimpasi shetani kujifananisha kwa sura yangu". Na maana yake: nikuwa shetani haiwezekani kwake kujifananisha na Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika umbile lake halisia, na vinginevyo anaweza kuja shetani na akasema kuwa yeye ndiye Mjumbe wa Mwenyezi Mungu na anakuwa katika umbile ambalo si umbile lake -Rehema na Amani ziwe juu yake-, huyu si Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- mtu atakapomuota mtu ndotoni na ikaingia hisia nafsini mwake kuwa huyu ndiye Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake-, basi hebu atafute sifa za huyu aliyemuona, je zinaendana na sifa za Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake au la? Ikiwa zitaendana: Basi atakuwa kamuona Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Na zisipoendana basi huyo si Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- bali hizi ni dhana toka kwa shetani kaziingiza katika nafsi ya huyu aliyelala kwamba ndiye Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- na wala si yeye Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake-, Na amepokea Imamu Ahmadi na Tirmidhiy katika shamaail: kutoka kwa Yazidi Al faarisiy amesema: Nilimuona Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ndotoni, nikasema kumwambia bin Abbas: Hakika mimi nimemuona Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ndotoni, akasema bin Abbasi: hakika Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alikuwa akisema: "Hakika shetani hawezi kujifananisha na mimi, basi atakayeniona mimi usingizini hakika atakuwa kaniona mimi", Je unaweza kueleza sifa za huyo bwana uliyemuota? Nikasema: Ndiyo: alipoeleza sifa zake, akasema bin Abbas: lau kama ungemuona ukiwa macho usingeweza kumsifia juu ya hapo" Na maana yake: nikuwa lau kama ungemuona Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ukiwa macho isingewezekana kumsifia zaidi ya hayo uliyomsifia, na hii maana yake nikuwa yeye alimuona Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake kweli.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama