عن أنس رضي الله عنه مرفوعاً: «من خَرج في طلب العلم فهو في سَبِيلِ الله حتى يرجع».
[حسن] - [رواه الترمذي]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake hadithi Marfu'u: "Yeyote atakayetoka katika kutafuta elimu basi huyo yuko katika njia ya Mwenyezi Mungu mpaka atakaporejea".
Ni nzuri - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Maana ya hadithi: Nikuwa atakayetoka nyumbani kwake au katika mji wake; kwaajili ya kutafuta elimu ya kisheria,huyo anakuwa katika hukumu ya aliyetoka kwaajili ya Jihadi katika njia ya Mwenyezi Mungu Mtukufu,mpaka atakaporudi kwa watu wake; kwasababu anakuwa ni kama mpiganaji katika kuihuisha kwake dini na kumdhalilisha shetani na kuitaabisha nafsi.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese German Kijapani Pashto Kiassam Albanian
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Nikuwa kutafuta elimu ni kupambana katika njia ya Mwenyezi Mungu.
  2. Mwenye kutafuta elimu ana malipo ya mpiganaji katika viwanja vya mapambano; kwasababu wote hao wanayasimamia yale yanayoweza kuipa nguvu sheria ya Mwenyezi Mungu na wanazuia yasiyokuwa humo.
  3. Ndani yake nikuwa mwenye kutoka katika kutafuta elimu atakuwa na malipo ya kutembea kwake na kwenda kwake na kurudi kwake mpaka atakaporejea kwa watu wake.