+ -

عن أبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«لَا يَحِلُّ لِامْرَأَةٍ مُسْلِمَةٍ تُسَافِرُ مَسِيرَةَ لَيْلَةٍ إِلَّا وَمَعَهَا رَجُلٌ ذُو حُرْمَةٍ مِنْهَا».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 1339]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake:
"Si halali kwa mwanamke wa kiislamu kusafiri mwendo wa usiku mmoja, isipokuwa awe pamoja na mwanaume mwenye uharamu wa kumuoa (ndugu yake)".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 1339]

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa ni haramu kwa mwanamke wa kiislamu kusafiri mwendo wa usiku mmoja isipokuwa awe pamoja na mwanaume katika maharimu wake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Amesema bin Hajari: Kutofaa kwa mwanamke kusafiri pasina maharim (ndugu), ni makubaliano ya wanachuoni isipokuwa katika Hija na Umra, na kutoka katika mji wa ushirikina, na wako waliolifanya hilo kuwa ni katika masharti ya Hija.
  2. Ukamilifu wa sheria ya Uislamu, na pupa yake juu ya kumlinda mwanamke na kumchunga.
  3. Kumuamini Mwenyezi Mungu na siku ya mwisho kunapelekea kunyenyekea sheria za Mwenyezi Mungu, na kusimama katika mipaka yake.
  4. Maharimu wa mwanamke ni mume wake au mtu wa haramu kwake kumuoa milele kwa sababu ya ukaribu wa kiukoo, au kunyonya, au ukwe, na anatakiwa awe muislamu, aliyebaleghe, mwenye akili timamu, mkweli, mwaminifu; kwa sababu lengo la maharimu ni kumlinda mwanamke na kumchunga na kusimamia mambo yake.
  5. Amesema Baihaqi: Kuhusu riwaya zilizokuja katika muda wa safari anaosafiri mwanamke ndani yake pamoja na maharimu: Na kilichopo nikuwa kila kinachoitwa safari mwanamke anakatazwa kusafiri pasina mume au maharimu, sawa sawa ziwe ni siku tatu au mbili au moja, au kaagizwa au kinginecho; kwa sababu ya riwaya ya bin Abbasi ambayo haikubagua, na ndio riwaya za mwisho za Imam Muslim zilizotangulia: "Asisafiri mwanamke isipokuwa awe pamoja na maharimu" Na hii inakusanya yote yanayoitwa safari. Mwisho, na hadithi hii ilikuwa kulingana na hali ya muulizaji na mji wake.