+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«مَنْ نَسِيَ وَهُوَ صَائِمٌ، فَأَكَلَ أَوْ شَرِبَ، فَلْيُتِمَّ صَوْمَهُ، فَإِنَّمَا أَطْعَمَهُ اللهُ وَسَقَاهُ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 1155]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake:
"Atakayesahau hali yakuwa kafunga akala au akanywa, basi atimize swaumu yake, kwani Mwenyezi Mungu kamlisha na kamnywesha".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 1155]

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa atakayekula au kunywa kwa kusahau akiwa kafunga swaumu ya faradhi au sunna basi atimize swaumu yake wala asifungue; kwa sababu hakukusudia kufungua, bali hiyo ni riziki Mwenyezi Mungu kamsogezea na akamlisha na kumnywesha.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kukubalika kwa swaumu ya aliyekula au kunywa kwa kusahau.
  2. Hana dhambi aliyesahau akala au kunywa; kwa sababu hilo si kwa maamuzi yake.
  3. Upole wa Mwenyezi Mungu kwa waja wake na kuwafanyia wepesi juu yao na kuwaondolea tabu na uzito juu yao.
  4. Hafungui mfungaji kwa chochote katika vile vyenye kufunguza ila zikikamilika sharti tatu: Ya kwanza: Awe anajua, akiwa mjinga hafungui, ya pili: Awe na kumbukumbu, kama kasahau swaumu yake ni sahihi na wala halazimiki kulipa, ya tatu: Iwe kwa hiari yake, na si kwa kulazimishwa, yaani atumie vyenye kufunguza kwa hiari yake mwenyewe.
Ziada