عن أبي سعيد الخُدْرِيِّ رضي الله عنه : أنه سمع النبي صلى الله عليه وسلم يقول: «إذا رأى أحدُكُم رُؤيا يُحِبُّهَا، فإنما هي من الله تعالى، فليَحْمَد الله عليها، وَلْيُحَدِّثْ بها - وفي رواية: فلا يُحَدِّثْ بها إلا من يُحَبُّ- وإذا رأى غير ذلك مِمَّا يَكْرَه، فإنما هي من الشيطان، فَلْيَسْتَعِذْ من شَرِّهَا، ولا يَذْكُرْهَا لأحد؛ فإنها لا تضره».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Saidi Al khudriy -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- yakwamba yeye alimsikia Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akisema: "Atakapoona mmoja wenu ndoto anayoipenda, basi hiyo imetoka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, na amshukuru Mwenyezi Mungu juu yake, na aisimulie- Na katika riwaya nyingine: asimsimulie yeyote ila yule anayempenda- Na akiota kinyume na hivyo miongoni mwa yale anayoyachukia, basi hayo yametokana na shetani, aombe kinga kutokana na shari yake, na asiyaeleze kwa yeyote; kwani hayo hayatoweza kumdhuru".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Atakapoona muislamu usingizini mwake yale yenye kumfurahisha, basi hiyo ni habari njema toka kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu, basi na amshukuru Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka kwa bishara hii njema, na asimsimulie yeyote isipokuwa yule anayempenda miongoni mwa familia yake au jirani zake au jamaa zake wale wema miongoni mwao, na akiota kinyume na hivyo miongoni mwa ndoto mbaya anazozichukia mandhari yake, au hapendi kujua ufafanuzi wake, basi hayo ni maigizo ya kishetani anayaleta shetani katika nafsi ya aliyelala usingizini mwake, ili amuhofishe na amuhuzunishe, basi akiona hivyo aombe kinga kwa Mwenyezi Mungu kutokana na shari zake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama