+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«مَنْ حَلَفَ فَقَالَ فِي حَلِفِهِ: وَاللَّاتِ وَالعُزَّى، فَلْيَقُلْ: لاَ إِلَهَ إِلَّا اللَّهُ، وَمَنْ قَالَ لِصَاحِبِهِ: تَعَالَ أُقَامِرْكَ، فَلْيَتَصَدَّقْ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 4860]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake-:
"Atakaye apa akasema katika kiapo chake: Na apa kwa Lata na uzza, basi aseme: Hapana apasaye kuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, na atakayesema kumwambia ndugu yake: Njoo tucheze kamari, basi na atoe sadaka".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح ابن حبان - 4860]

Ufafanuzi

Anatahadharisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuapa kwa jina la asiyekuwa Mwenyezi Mungu; kwani muumini haapi ila kwa Mwenyezi Mungu, Na anaeleza kuwa atakayeapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu; Kwa mfano mtu akiapa kwa Lata na Uzza - masanamu mawili yaliyokuwa yakiabudiwa katika zama za kabla ya Uislamu - basi aseme ndani ya nafsi yake: Hapana apasayekuabudiwa kwa haki isipokuwa Mwenyezi Mungu, ili ajiepushe na ushirikina na ili iwe ni fidia ya kiapo chake hicho.
Kisha akaeleza rehema na amani ziwe juu yake kuwa atakayemwambia rafiki yake: Njoo tucheze kamari - ambayo ni watu wawili au zaidi watakaposhindana kwa sharti kuwa baina yao kuna pesa ambayo mshindi ataichukua, na kila mmoja wao lazima ima apate hasara au faida-; ni sunna atoe sadaka kwa kitu chochote kama kafara ya yale aliyoyahamasisha.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Pashto Kiassam الأمهرية الهولندية الغوجاراتية النيبالية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kiapo hakiwi isipokuwa kwa Mwenyezi Mungu na majina yake na sifa zake.
  2. Kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu ni haramu, ama kuapa kwa masanamu kama Lata au Uzza au kuapia amana, au kuapa kwa Mtume au kitu kingine chochote.
  3. Amesema Khattwabi: Kiapo kinakuwa kwa Muabudiwa Mtukufu, basi akiapa kwa Lata na mfano wa hayo anakuwa kawaiga makafiri, basi akaamrishwa kukirekebisha kwa neno la tauhidi.
  4. Mwenye kuapa kwa asiyekuwa Mwenyezi Mungu si lazima atoe kafara ya kiapo chake, bali anatakiwa kutubia na kuomba msamaha, kwa sababu hilo ni kubwa mno kuliko kusamehewa na kisichokuwa toba.
  5. Kumeharamishwa kamari kwa aina zake zote na mitindo yake yote, ambayo ni kamari aliyoiharamisha Mwenyezi Mungu Mtukufu na akaiambatanisha na pombe na masanamu.
  6. Ulazima wa kurudi na kuacha maasi wakati wa kuyafanya.
  7. Atakayefanya jambo baya anatakiwa afuatishe jambo jema; kwa sababu matendo mema huondoa maovu.