+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رضي الله عنه قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«اثْنَتَانِ فِي النَّاسِ هُمَا بِهِمْ كُفْرٌ: الطَّعْنُ فِي النَّسَبِ، وَالنِّيَاحَةُ عَلَى الْمَيِّتِ».

[صحيح] - [رواه مسلم] - [صحيح مسلم: 67]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira radhi za Allah ziwe juu yake amesema: Amesema Mtume rehema na amani ziwe juu yake:
"Mambo mawili kwa watu hayo kwao ni ukafiri: Kutiana doa katika nasaba (ukoo), na kulia kwa kumuomboleza maiti".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Imamu Muslim]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuhusu mambo mawili kwa watu kuwa ni katika matendo ya makafiri, na ni tabia za enzi za ujinga, nayo ni:
La kwanza: Kutukana nasaba (koo) za watu na kuzishushia heshima na kujikweza juu yao.
La pili: Kunyanyua sauti wakati wa msiba kwa kulalamika juu ya kadari, au kukata nguo kwa sababu ya mfadhaiko mkubwa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Himizo la unyenyekevu na kutokujikweza kwa watu
  2. Ulazima wa kusubiri juu ya msiba na kutolalamika.
  3. Matendo haya ni katika ukafiri mdogo, na si kwamba mwenye kufanya sehemu katika sehemu za ukafiri anakuwa kafiri ukafiri unaomtoa mtu katika mila ya Uislamu mpaka umthibitikie ukafiri mkubwa.
  4. Uislamu umekataza mambo yote yanayopelekea kutengana baina ya waislamu kama kutukana nasaba na mengineyo.