عن عُقْبَة بن عامر رضي الله عنه قال: قلت: يا رسول الله ما النَّجَاة؟ قال: «أَمْسِكْ عليك لِسَانَكَ، وَلْيَسَعْكَ بَيتُك، وابْكِ على خَطِيئَتِكَ».
[صحيح] - [رواه الترمذي وأحمد]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ukbah bin Aamir -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Nilisema ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu ni kupi kusalimika? Akasema: "Zuia ulimi wako, na ikutosheleze nyumba yako, na ulie juu ya makosa yako"
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Tirmidhiy

Ufafanuzi

Katika hadithi hii: Ukbah bin Aamir -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- alimuuliza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- Yale yatakayomuokoa Akhera, Na hili ndilo lengo la kila muislamu mwenye pupa na Akhera yake. Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- akasema kumwambia: "Zuia ulimi wako" Alimuelekeza Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- ashike ulimi wake; na hiyo ni kwasababu ya ukubwa wa hatari yake na wingi wa madhara yake, ikawa ni wajibu kwa muislamu kuzuia ulimi wake, na apendelee kunyamaza zaidi kuliko kuzungumza isipokuwa katika yale yenye manufaa na Akhera. "Na ikutosheleze nyumba yako" Yaani mtu akae nyumbani kwake, na asitoke ila kwa dharura, na asikereke kukaa ndani yake, bali aifanye kuwa ni sehemu ya kufaidika, kwani hiyo ni sababu ya kuepukana na shari na fitina. "Na ulie juu ya madhambi yako" Yaani: lia ukiweza, ukijuta kwa maasi yako, na utubie kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu katika yale yaliyotokea kwako, kwani hakika Mwenyezi Mungu Mtukufu anakubali toba ya waja wake na anasamehe makosa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama