عن ابن عمر رضي الله عنهما أن رسول الله صلى الله عليه وسلم قال: «إذا أَكَلَ أحدُكم فَلْيَأْكُلْ بِيَمِينِه، وإذا شَرِب فَلْيَشْرَبْ بِيَمِينِه فإنَّ الشيطان يأكلُ بِشِمَالِه، ويَشْرَب بِشِمَالِه».
[صحيح] - [رواه مسلم]
المزيــد ...
Kutoka kwa Bin Omar Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Yakwamba Mjumbe wa Mwenyezi Mungu -Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakapo kula mmoja wenu basi na ale kwa mkono wake wa kulia, na atakapo kunywa basi na anywe kwa mkono wake wa kulia, kwani shetani anakula kwa mkono wako wake wa kushoto, na anakunywa kwa mkono wake wa kushoto".
Sahihi - Imepokelewa na Imamu Muslim
Hadithi hii ndani yake kuna amri ya kula kwa mkono wa kulia, na kunywa kwa mkono wa kulia; na katazo la kula na kunywa kwa mkono wa kushoto, na kumebainishwa sababu ya hukumu hii, nayo nikuwa shetani anakula na kunywa kwa mkono wake wa kushoto, na inaonyesha pia kuwa amri hapa ni ya kuwajibisha, nakuwa kula na kunywa kwa mkono wa kushoto ni haramu, kwasababu yeye katoa sababu kuwa hicho ni kitendo cha shetani na ni tabia yake, na muislamu ameamrishwa kujiepusha na njia za watu waovu, achilia mbali shetani, na atakayejifananisha na watu fulani basi na yeye ni miongoni mwao.