عن عمر بن أبي سلمة قال: كنتُ غُلاما في حَجْرِ رسول الله صلى الله عليه وسلم ، وكانتْ يَدِي تَطِيشُ في الصَّحْفَة، فقالَ لِي رسول الله صلى الله عليه وسلم : «يا غُلامُ، سمِّ اَلله، وكُلْ بِيَمِينِك، وكُلْ ممَّا يَلِيكَ» فما زَالَتْ تِلك طِعْمَتِي بَعْدُ.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Omar bin Abii Salama Amesema: Nilikuwa kijana katika malezi ya Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, na ulikuwa mkono wangu ukizunguka pande zote katika sahani (ya chakula) Akasema kuniambia mimi Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake: "Ewe kijana, mtaje Mwenyezi Mungu, na ule kwa mkono wako wa kulia, na ule chakula kilichopo mbele yako" kinachokuelekea" Basi sikuacha tena kula kama nilivyoelekezwa baada ya hapo.
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Alikuwa Omar bin Abii Salama- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- ni mtoto wa mke wa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Ummu salama -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake-; Na alikuwa chini ya malezi yake na uangalizi wake, na ameeleza miongoni mwa hali zake katika hadithi hii, kwamba yeye alikuwa akiutembeza mkono wake katika pande zote za sahani ili achukue chakula, akamfundisha Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake katika hadithi hii adabu tatu miongoni mwa adabu za chakula: Ya kwanza: Ni kusema "Bismillaah" -kwa jina la Mwenyezi Mungu" mwanzo wa kula. Na ya pili: Ni kula kwa mkono wa kulia. Na ya tatu ni kula kinachomuelekea; kwasababu kula kwake sehemu ya mkono wa mwenzie ni utovu wa adabu, Wamesema wanachuoni: Ispokuwa kama chakula kitakuwa aina tofauti tofauti, Mfano kama biringanya nyama na kadhalika, hakuna ubaya ukavuka mkono wako kufuata aina hii au ile, pamoja na kula kinachomuelekea katika aina ile, na vilevile atakapokuwa mtu anakula peke yake hakuna tatizo akila upande mwingine; kwasababu hakuna yeyote atakayemuudhi katika hilo.