+ -

عن عبد الله بن عمر رضي الله عنهما قال:
لعن النبي صلى الله عليه وسلم الوَاصِلَةَ والمُسْتَوْصِلَةَ، والوَاشِمَةَ والمُسْتَوشِمَةَ.

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح البخاري: 5947]
المزيــد ...

Imepokewa kutoka kwa Abdallah bin Omari -radhi za Allah ziwe juu yake yeye na baba yake- amesema:
Kamlaani Mtume rehema na amani ziwe juu yake mwenye kuunga nywele na mwenye kuungwa, na mwenye kuchora chata na mwenye kuchorwa.

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح البخاري - 5947]

Ufafanuzi

Dua ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake ya kulaaniwa na kufukuzwa na kuwekwa mbali na rehema ya Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa makundi ya aina nne: La kwanza: Mwanamke mwenye kuunga nywele zake au za mwenzake kwa nywele zingine. La pili: Na mwenye kutaka kuungwa nywele, kwa kumuomba mwenzake amuunganishe nywele zake kwa nywele zingine. La tatu: Mwenye kupiga chata, na anayejichoma sindano katika sehemu ya mwili wake, kama uso au kiganja au kifua, na kuweka wanja au mfano wake, ili kubakie alama ya bluu, au kijani; kwa kutaka kujipamba au uzuri. La nne: Mwenye kutaka kupigwa chata, ni yule anayeomba kupigwa chata. Na matendo haya ni katika madhambi makubwa.

Katika Faida za Hadithi

  1. Amesema bin Hajari: Ni kwamba linalozuiwa katika hilo kuunga nywele kwa nywele, na ama akiunga nywele kwa kitu kingine kisichokuwa nywele kama kitambaa au kinginecho haitoingia katika katazo.
  2. Katazo la kusaidizana katika madhambi.
  3. katazo la kubadili umbile la Mwenyezi Mungu; kwa sababu kufanya hivyo ni udanganyifu na ni ghushi.
  4. Kufaa kumlaani aliyelaaniwa na Mwenyezi Mungu na Mtume wake kwa mfumo wa ujumla.
  5. Inaingia katika kuunga nywele katika zama zetu hizi kuvaa mawigi, nalo ni jambo la haramu, kwakuwa kuna kujifananisha na makafiri na udanganyifu na ghushi na uongo.
  6. Amesema Khattwabi: Hakika imekuja ahadi ya adhabu kali katika mambo haya; kwakuwa ndani yake kuna ghushi na udanganyifu, na lau lingeruhusiwa lolote katika haya ingelikuwa njia ya kuhalalisha mengine katika aina za ghushi, na kwakuwa ndani yake kuna kubadili maumbile, na katika hilo kuna ishara ya hadithi ya bin Masudi kwa kauli yake: "Wenye kubadili maumbile ya Mwenyezi Mungu", na Allah ndiye mjuzi zaidi.
  7. Amesema Nawawi: Nalo ni jambo la haramu kwa mfanyaji na mwenye kufanyiwa, na sehemu aliyochorwa inakuwa najisi, ikiwa ataweza kuiondoa kwa tiba basi ni wajibu kwake kufanya hivyo na isipowezekana basi aiondoa kwa upasuaji, ikiwa atahofia kuharibika au kukosa kiungo au matumizi yake au chochote kibaya katika kiungo kinachoonekana basi haitokuwa wajibu kwake kuiondoa, na akitubia hatobaki na madhambi, na asipohofia chochote katika hayo basi ni lazima kwake, na atakuwa ameasi akichelewesha kuiondoa. Mwisho.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kikurdi Kihausa Kireno Kiassam الهولندية الغوجاراتية الرومانية المجرية الجورجية
Kuonyesha Tarjama