+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضِيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«لَا تَمْنَعُوا إِمَاءَ اللَّهِ مَسَاجِدَ اللَّهِ، وَلَكِنْ لِيَخْرُجْنَ وَهُنَّ تَفِلَاتٌ».

[حسن] - [رواه أبو داود] - [سنن أبي داود: 565]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Msiwazuie vijakazi wa Mwenyezi Mungu kwenda katika misikiti ya Mwenyezi Mungu, lakini wakitaka kutoka watoke wakiwa hawajajipamba".

[Ni nzuri] - [Imepokelewa na Abuu Daud] - [سنن أبي داود - 565]

Ufafanuzi

Amemkataza Mtume rehema na amani ziwe juu yake msimamizi wa mwanamke na muhusika wake kuwakataza wanawake kwenda Msikitini, na akawaamrisha wanawake wakati wa kutoka kwenda Msikitini watoke bila kujipuliza manukato na wasitoke kwa kujiachia kwa mapambo; ili wasiwe sababu ya fitina kwa wanaume.

Katika Faida za Hadithi

  1. Kumpa ruhusa mwanamke ya kwenda kuswali Msikitini atapokuwa na uhakika wa kutopata fitina, na akatoka bila mapambo wala manukato.
  2. Wameitumia hadithi hii kama ushahidi kuwa mwanamke hatoki nyumbani kwake isipokuwa kwa idhini yake, kwakuwa amri ya idhini imeelekezwa kwa wanaume.
  3. Uislamu umewapa kipaumbele wanawake, na kutowazuia kwa mambo ambayo yanaweza kuwa ni heri kwao kama kutoka kwenda kutafute elimu na mfano wake.
  4. Kuthibiti kwa usimamizi wa mwanaume juu ya mwanamke na kumchunga.
Tafsiri: Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kivetenamu Kikurdi Kireno Thai Kiassam الهولندية الدرية المجرية الجورجية المقدونية
Kuonyesha Tarjama