+ -

عَنْ أَبِي هُرَيْرَةَ رَضيَ اللهُ عَنْهُ أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللَّهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«إِذَا دَخَلَ أَحَدُكُمْ المَسْجِدَ فَلْيُسَلِّمْ عَلَى النَّبِيِّ وَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ افْتَحْ لِي أَبْوَابَ رَحْمَتِكَ، وَإِذَا خَرَجَ فَلْيُسَلِّمْ عَلَى النَّبِيِّ وَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ اعْصِمْنِي مِنْ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ»، وَلِلْحَاكِمِ: «وَإِذَا خَرَجَ فَلْيُسَلِّمْ عَلَى النَّبِيِّ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ وَلْيَقُلْ: اللَّهُمَّ أَجِرْنِي مِنَ الشَّيْطَانِ الرَّجِيمِ».

[حسن] - [رواه ابن ماجه والحاكم] - [سنن ابن ماجه: 773]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Abuu Huraira -radhi za Allah ziwe juu yake- yakwamba Mtume -rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Atakapoingia mmoja wenu Msikitini basi amtakie rehema Mtume kisha aseme: Allaahummaf-tahlii abwaaba rahmatika, (Ewe Mwenyezi Mungu nifungulie milango ya rehema zako), na akitoka amtakie rehema Mtume na aseme: Allaahumma'swimnii minash-shaitwaanir-rajiim", (Ewe Mwenyezi Mungu nikinge dhidi ya Shetani aliyelaaniwa. Na katika riwaya ya Al-Haakim: "Na akitoka amtakie rehema Mtume rehema na amani ziwe juu yake na aseme: Ewe Mwenyezi Mungu nilinde dhidi ya Shetani aliyelaaniwa".

[Ni nzuri] - [رواه ابن ماجه والحاكم] - [سنن ابن ماجه - 773]

Ufafanuzi

Amemuelekeza Mtume rehema na amani ziwe juu yake Muislamu atakapotaka kuingia Msikitini amtakie rehema Mtume rehema na amani ziwe juu yake kwa kusema: Allaahumma swalli alaa Muhammadi, kisha aseme: "Ewe Mwenyezi Mungu nifungulie milango ya rehema zako". Na akitoka amtakie rehema Mtume na aseme: "Ewe Mwenyezi Mungu nikinge na shetani aliyelaaniwa", na katika riwaya nyingine ya imamu Hakim: Na aseme: "Awe Mwenyezi Mungu nilinde na Shetani aliyelaaniwa".

Katika Faida za Hadithi

  1. Sunna ya kusoma dua hii wakati wa kuingia Msikitini na wakati wa kutoka.
  2. Dua hii ni kwa misikiti yote, hata Msikiti mtukufu wa Makka.
  3. Rehema zimetajwa maalumu wakati wa kuingia, na kukingwa na Shetani wakati wa kutoka: Ni kwakuwa mwenye kuingia anashughulika na kile kinachomuweka karibu na Mwenyezi Mungu na karibu na Pepo yake ikawa ni mahala pazuri pa kutaja rehema, na akitoka anakwenda katika dunia na yote yaliyomo miongoni mwa mapumbao na vyenye kushughulisha, ikawa ni sehemu nzuri ya kuomba ulinzi kutoka kwa Mwenyezi Mungu na kuhifadhiwa kutokana na Shetani.
Tafsiri: Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kivetenamu Kikurdi Kireno Thai Kiassam الهولندية الدرية المجرية الجورجية المقدونية
Kuonyesha Tarjama