عن أنس بن مالك رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «سَوُّوا صُفُوفَكُم، فإِنَّ تَسوِيَة الصُّفُوف من تَمَام الصَّلاَة».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Anas bin Malik- Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Allah- Rehema na amani ziwe juu yake- "Nyoosheni safu zenu, kwani hakika kunyoosha safu ni katika ukamilifu wa swala".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anauelekeza Nabii -Rehema na Amani ziwe juu yake- umma wake katika yale ambayo ndani yake kuna kutengemaa kwao na kufaulu kwao, basi yeye hapa anawaamrisha wanyooshe safu zao, kiasi kwamba iwe alama yao upande wa kibla ni moja, na wazibe nyufa za safu, mpaka kusiwe kwa shetani na njia ya kuichezea swala yao, na akawaelekeza -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika baadhi ya faida ambazo wanazipata kutokana na kurekebisha safu, na hii ni kwasababu kuzirekebisha ni alama ya kutimia kwa swala na kukamilika kwake, nakuwa kupinda kwa safu ni tatizo na ni mapungufu ndani yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno الدرية
Kuonyesha Tarjama