+ -

عن أنس بن مالك رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «سَوُّوا صُفُوفَكُم، فإِنَّ تَسوِيَة الصُّفُوف من تَمَام الصَّلاَة».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Anas -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -Rehema na amani ziwe juu yake:
"Nyoosheni safu zenu, kwani hakika kunyoosha safu ni katika ukamilifu wa swala"

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Anawaamrisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake wenye kuswali kunyoosha safu zao, na wasitanguliane wala wasirudi nyuma, na kwamba kuzinyoosha ni sehemu ya kukamilisha na ukamilifu wa Sala, na kuwa kupinda kwa safu ni dosari na ni upungufu ndani yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Thai Kiassam السويدية الأمهرية القيرقيزية اليوروبا الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Sheria ya kuchunga kila kinachokamilisha swala na kuiweka mbali na upungufu.
  2. Hekima ya Mtume rehema na amani ziwe juu yake katika kufundisha, kwani aliihusisha hukumu na sababu yake; ili iwe wazi hekima ya kuletwa sheria hiyo, na nafsi ipate hamasa ya kuitekeleza.