+ -

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضيَ اللهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«مَنْ صَلَّى صَلاَتَنَا وَاسْتَقْبَلَ قِبْلَتَنَا وَأَكَلَ ذَبِيحَتَنَا فَذَلِكَ المُسْلِمُ الَّذِي لَهُ ذِمَّةُ اللَّهِ وَذِمَّةُ رَسُولِهِ، فَلاَ تُخْفِرُوا اللَّهَ فِي ذِمَّتِهِ».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 391]
المزيــد ...

Imepokelewa kutoka kwa Anas bin Maliki -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume -rehema na amani ziwe juu yake:
"Atakayeswali swala yetu na akaelekea kibla chetu na akala kichinjwa chetu basi huyo ni Muislamu mwenye dhima ya Mwenyezi Mungu na dhima ya Mtume wake, msimfanyie hiana Mwenyezi Mungu katika dhima yake".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 391]

Ufafanuzi

Ameeleza Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa atakayeshikamana na nembo za dini za wazi akaswali mfano wa swala yetu, na akaelekea upande wa Ka'aba Kibla yetu, na akala kichinjwa chetu kwa kuamini kuwa ni halali; basi huyu ndio Muislamu ambaye anadhima ya Mwenyezi Mungu na Mtume wake na ahadi yake, msitengue amani ya Mwenyezi Mungu na ahadi yake ndani yake.

Katika Faida za Hadithi

  1. Amesema bin Rajab: Hadithi imeonyesha kuwa damu haikingwi tu kwa mtu kutoa shahada mbili, mpaka atekeleze haki zake, na haki yake yenye mkazo zaidi ni swala; na ndio maana ameitaja pekee, na katika hadithi nyingine ameongeza swala na zaka.
  2. Mambo ya watu huchukuliwa kwa dhahiri pasina undani, atakayedhihirisha nembo za dini basi zitatekelezwa kwake hukumu za Waislamu madamu hajadhihirisha kinyume na hivyo.
  3. Amesema bin Rajab: Ametaja kuelekea kibla kama ishara yakuwa ni lazima kuitekeleza swala ya Waislamu iliyowekwa kisheria ndani ya kitabu chao kilichoteremshwa kwa Nabii wao, nayo ni swala ya kuelekea kibla, na vinginevyo atakayeswali kwa kuelekea Palestina baada ya kufutwa kwake kama Mayahudi au Mashariki kama Wakristo, huyo si Muislamu, hata kama atashuhudia kwa shahada ya kumpwekesha Mwenyezi Mungu.
  4. Hapa kuna dalili ya utukufu wa kuelekea kibla katika swala, kwa sababu hakutaja katika sharti za swala sharti nyingine, kama twahara na nyinginezo.
  5. Amesema bin Rajab: Kutaja kula kichinjwa cha Waislamu kuna ishara kuwa ni lazima kushikamana na sheria zote za Uislamu za wazi, na miongoni mwa kubwa zake ni kula kichinjwa cha Waislamu, na kukubaliana nao katika kichinjwa chao, atakayekataa kula huyo si Muislamu.
Tafsiri: Lugha ya Kiindonesia Kibangali Kivetenamu Kikurdi Kireno Thai Kiassam الهولندية الدرية المجرية الجورجية المقدونية
Kuonyesha Tarjama