عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما مرفوعاً: قال: لم يكن رسول الله صلى الله عليه وسلم فاحشاً ولا متفحشاً، وكان يقول: «إن من خياركم أحسنكم أخلاقًا».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Na kutoka kwa Abdillahi Bin Amriy bin Aaswi- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Hadithi Marfu'u- Amesema: "Hakuwa Mtume rehema na Amani zimfikie Muovu, wala mwenye kutaka machafu" Na alikuwa akisema: "Hakika katika wabora wenu ni mzuri wenu kitabia"
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hakuwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- mwenye kauli mbovu, wala vitendo vibaya, wala mwenye kukusudia kufanya hayo, mwenye kujilazimisha kwa hayo, bali alikuwa mwenye tabia tukufu, na akaeleza kuwa muumini bora ni yule mwenye tabia njema kati yao, kwasababu tabia njema inapelekea katika matendo mazuri na kuacha maovu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ni wajibu kwa muumini ajiweke mbali na maneno mabaya na vitendo viovu.
  2. Alijikaza Mtume wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake katika tabia zake kiasi kwamba halikutokea kwake ispokuwa jambo jema na kauli njema.
  3. Tabia njema ni uwanja wa kushindania kati ya waumini, atakayeshinda hapo basi atakuwa ni mbora wa waumini na mkamilifu wao kiimani.