عن أبي مسعود البدري رضي الله عنه مرفوعاً: «إذا أَنْفَقَ الرجلُ على أهله نَفَقَةً يَحْتَسِبُهَا فهي له صَدَقَةٌ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Mas'udi Al-Badriy- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Hadithi Marfu'u: "Atakapotoa mtu kwa familia yake tumizi lolote akitaraji malipo basi hilo kwake ni sadaka".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Atakapotoa mtu kwa watu wake ambao inamlazimu kuwahudumia kama mke wake na mtoto wake, na wengineo hivyo hivyo, naye akikusudia kujikaribisha kwa Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa hilo na akitaraji malipo kwa kile anachokitoa, basi yeye analipwa kwa tumizi hilo kama malipo ya sadaka kwa mafakiri na mfano wao katika njia za wema.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kupatikana malipo na thawabu kwa kutoa katika familia. Muumini anatafuta katika amali yake radhi za Mwenyezi Mungu na yale yaliyoko kwake katika malipo na thawabu.