عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «مَنْ قَالَ: سُبْحَانَ اللَّهِ وَبِحَمْدِهِ في يومٍ مِائَةَ مَرَّةٍ حُطَّتْ عَنْهُ خَطَايَاهُ وَإِنْ كَانَتْ مِثْلَ زَبَدِ الْبَحْرِ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake, Amesema: "Atakayesema: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema ni zake- kwa siku mara mia moja, atasamehewa makosa yake hata kama yatakuwa mfano wa povu la bahari".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Katika hadithi kuna dalili juu ya fadhila za dhikiri hii iliyokusanya kumtukuza Mwenyezi Mungu kwa namna hii, nakuwa atakayeileta hiyo hakika Mwenyezi Mungu atamfutia madhambi yake vyovyote yatakavyokuwa mengi, hata kama yatafikia mfano wa povu la bahari katika wingi, ni fadhila kutoka kwa Mwenyezi Mungu kwa waja wake wenye kumtaja. Nayo ni katika nyiradi za asubuhi kwa kile kilicho elezwa katika hadithi: "Katika siku" na ni katika nyiradi za jioni pia, kwa hadithi ya Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mjumbe wa Mwenyezi Mungu Rehema na Amani ziwe juu yake: "Atakayesema wakati ameamka na wakati ameshinda: Sub-haana llaahi wabihamdihi- Ametakasika Mwenyezi Mungu na sifa njema ni zake- mara mia moja, hatokuja yeyote siku kiyama na kitu bora kuliko alichokuja nacho, ispokuwa mtu aliyesema kama alivyosema au akazidisha" kaipokea Muslim.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa nyiradi ambazo zimekusanya kumtukuza Mwenyezi Mungu Mtukufu, na kumtakasa na yale yasiyoendana nayo katika mapungufu na aibu.
  2. Uwazi wa hadithi unaonyesha kuwa malipo haya yanapatikana kwa atakayesema ndani ya siku, sawa sawa ameyasema kwa mfululizo au kwa kuyaachanisha, au baadhi yake mchana na baadhi yake mwisho wa usiku.
  3. katika kauli yake: (Atakayesema:.) Ni jibu kwa mwenye kusema kuwa mja kalazimishwa juu ya matendo yake na wala hana maamuzi.