عن أبي هريرة رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم فيما يَحْكِي عن ربه تبارك وتعالى، قال: «أَذْنَبَ عَبْدٌ ذَنْبًا، فقال: اللهم اغْفِرْ لي ذَنْبِي، فقال اللهُ تبارك وتعالى: أَذْنَبَ عَبْدِي ذَنْبًا، فَعَلِمَ أَنَّ له رَبًّا يَغْفِرُ الذَّنْبَ، ويَأْخُذُ بالذَّنْبِ، ثم عَادَ فَأَذْنَبَ، فقال: أَيْ رَبِّ اغْفِرْ لي ذَنْبِي، فقال تبارك وتعالى: أَذْنَبَ عَبْدِي ذَنْبًا، فَعَلِمَ أَنَّ له رَبًّا، يَغْفِرُ الذَّنْبَ، ويَأْخُذُ بالذَّنْبِ، قَدْ غَفَرْتُ لِعَبْدِي فَلْيَفْعَلْ ما شَاءَ»
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abuu Huraira Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- katika yale anayoyasimulia kutoka kwa Mola wake Aliyetakasika na kutukuka, Amesema: "Ametenda dhambi mja, akasema: Ewe Mola wangu nisamehe mimi dhambi langu, akasema Mwenyezi Mungu Aliyetakasika na kutukuka: Mja wangu katenda dhambi, na akajua kuwa ana Mola anayesamehe dhambi, na analichukua dhambi, kisha akarudia akatenda dhambi, na akasema: Ewe Mola wangu nisamehe mimi dhambi langu, Akasema Aliyetakasika na kutukuka: Mja wangu katenda dhambi, na akajua kuwa ana Mola anayesamehe dhambi, na analichukua dhambi, basi hakika nimemsamehe mja wangu na afanye atakavyo".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Atakapofanya mja dhambi, kisha akasema: Ewe Mola wangu nisamehe mimi dhambi langu, anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: kafanya mja wangu dhambi, na akajua kuwa yeye ana Mola anayesamehe dhambi, akamsitiri na akaliachilia mbali, au akamuadhibu juu yake, kisha akarudi akatenda dhambi tena, Akasema: Ewe Mola wangu nisamehe mimi dhambi langu, anasema Mwenyezi Mungu Mtukufu: kafanya mja wangu dhambi, na akajua kuwa yeye ana Mola anayesamehe dhambi, akamsitiri na akaliachilia mbali, au akamuadhibu juu yake, basi hakika nimemsamehe mja wangu, basi na afanye ayatakayo katika madhambi na ayafuatishe na toba sahihi, madamu ataendelea kufanya hivi, anafanya dhambi anatubia ninamsamehe, kwani toba inabomoa yaliyo kabla yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ukubwa wa fadhila za Mwenyezi Mungu na rehema zake juu ya waja wake madamu bado wanaendelea kuamini kuwa Mola wao mkononi mwake kuna mamlaka yao, akitaka anasamehe na akitaka anaadhibu.
  2. Toba sahihi inafuta madhambi.
  3. Mwenye kumuamini Mwenyezi Mungu Mtukufu unasafishika moyo wake kwa toba na anatumaini msamaha wa Mola wake, akafanya haraka kutengeneza na kufanya mambo ya kheri, na likitokeza kwake dhambi anajirudi nafsini mwake kwa toba, na haendelei na maasi.
  4. Laiti likijirudia dhambi kwa mja mara mia moja au zaidi na akatubia katika kila mara, itakubaliwa toba yake na litadondoka dhambi lake, na hata akitubia kwa yote kwa toba moja baada ya yote pia itakuwa sawa toba yake.