+ -

عن أبي أيوب رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال:
«مَنْ قَالَ: لَا إِلَهَ إِلَّا اللهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ وَلَهُ الْحَمْدُ وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ، عَشْرَ مِرَارٍ كَانَ كَمَنْ أَعْتَقَ أَرْبَعَةَ أَنْفُسٍ مِنْ وَلَدِ إِسْمَاعِيلَ».

[صحيح] - [متفق عليه] - [صحيح مسلم: 2693]
المزيــد ...

Imepokelewa Kutoka kwa Abuu Ayub -Radhi za Allah ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- amesema:
"Atakayesema: Laa ilaaha illa llaahu wahdahu Laa shariika lahu, Lahul-Mulku walahul hamdu Wahuwa a'laa kulli shai-in qadiir, mara kumi (10) atakuwa ni kama aliyewaacha huru watu wanne katika wana wa Ismail".

[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim] - [صحيح مسلم - 2693]

Ufafanuzi

Anaeleza Mtume -Rehema na amani ziwe juu yake- kuwa atakayesema: "Laa ilaaha illa llaahu wahdahu Laa shariika lahu, Lahul-Mulku walahul hamdu Wahuwa a'laa kulli shai-in qadiir", na maana yake nikuwa: Hakuna anayestahiki kuabudiwa kwa haki isipokuwa Allah peke yake asiye na mshirika, nakuwa Yeye Mtukufu amepwekeka kwa Ufalme uliotimia, na mwenye kustahiki kutajwa na sifa na mapenzi na kutukuzwa pasina mwingine asiyekuwa Yeye, nakuwa Yeye ni muweza hakuna chochote kinachomshinda. Atakayeirejea rejea dhikiri hii tukufu kwa siku mara kumi (10); Basi atakuwa kapata malipo mfano wa malipo ya atakayeondoa utumwa kwa watumwa wanne katika watoto wa Ismail bin Ibrahim -Amani iwe juu yao-, na ametaja kizazi cha Ismail -Amani iwe juu yake-; kwa sababu wao ndio watukufu zaidi kuliko wengine.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Ki ighori Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية Luqadda qer-qeesiya النيبالية Luqadda yuruuba الليتوانية الدرية الصربية الصومالية Luqadda kiniya ruwadiga الرومانية المجرية التشيكية Luqadda malgaashka Kiitaliano Luqadda kinaadiga Luqadda Asariga الأوكرانية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa dhikiri hii iliyokusanya kumpwekesha Mwenyezi Mungu Mtukufu kwa Uungu, na Ufalme, na sifa njema, na uwezo uliotimia.
  2. Thawabu hizi anazipata atakayesema kwa mfululizo au tofauti tofauti.