عن أبي أيوب رضي الله عنه عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «مَنْ قَالَ: لَا إلَهَ إلَّا اللَّهُ وَحْدَهُ لَا شَرِيكَ لَهُ، لَهُ الْمُلْكُ، وَلَهُ الْحَمْدُ، وَهُوَ عَلَى كُلِّ شَيْءٍ قَدِيرٌ عَشْرَ مَرَّاتٍ كَانَ كَمَنْ أَعْتَقَ أَرْبَعَةَ أَنْفُسٍ مِنْ وَلَدِ إسْمَاعِيلَ».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Abii Ayubu- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kutoka kwa Mtume Rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Atakayesema: Laa ilaaha illa llaahu wahdahu Laa shariika lahu, Lahul Mulku walahul Hamdu, Wahuwa a'laa kulli shay in Qadiir (Hapana Mola ispokuwa Mwenyezi Mungu, yeye pekee asiye na mshirika, Ufalme ni wake, na sifa njema ni zake, Naye juu ya kila kitu ni muweza), akasema hivyo mara kumi, Atakuwa sawa na aliyeacha huru nafsi nne katika watoto wa Ismail".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Hadithi hii ni dalili juu ya ubora wa kumtaja Mwenyezi Mungu kwa yale yaliyomo miongoni mwa kukiri Tauhidi (kumpwekesha Mwenyezi Mungu), nakuwa atakayesema mara kumi kwa kujua maana yake na kwa kufanyia kazi malengo yake atakuwa na malipo mfano wa malipo ya aliyeacha huru watumwa wanne kutoka katika kizazi cha Ismail bin Ibrahim -Ziwe juu yao sala na salamu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Ubora wa dhikiri hii inayoambatana na neno la kumpwekesha Mwenyezi Mungu ambalo ndio msingi wa uislamu.
  2. Kupwekeka kwake Aliyetakasika na kutukuka kwa Uungu na Ufalme na sifa njema.
  3. Katika faida za hadithi: Nikuwa Mwenyezi Mungu ana ufalme wa moja kwa moja, na sifa za moja kwa moja, nakuwa uwezo wake ni kwa kila kitu.
  4. Nikuwa katika dhikiri hii hakuna ziada ya "Yuhyii Wayumiitu" ana huisha na kufisha.
  5. Kauli yake katika hadithi "Mara kumi" kwa uwazi wake inaonyesha kuwa hakuna tofauti kati ya kuileta mfululizo au kwa kuikatishakatisha.
  6. Katika hadithi kuna kufaa kuwa baadhi ya waarabu kuwa watumwa pale zikiwapitia sababu za kuwa watumwa.
  7. Ubora wa waarabu juu ya wengine, kwasababu wao ndio watoto wa Ismail.