عن معاوية بن أبي سفيان رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «من يُرِدِ الله به خيرا يُفَقِّهْهُ في الدين».
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...
Kutoka kwa Muawiya bin Abii Sufiyani- Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake Amesema: Amesema Mtume Rehema na Amani zimfikie: "Mwenye kumtakia Mwenyezi Mungu kheri kwake humpa ufahamu katika dini".
Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim
Mwenye kumtakia Mwenyezi Mungu kwake manufaa na kheri anamfanya kuwa mtambuzi wa hukumu za kisheria mwenye maarifa ndani yake, Na Ufahamu una maana mbili: wa kwanza: kuzijua hukumu za kisheria za kielimu kutoka katika dalili zake zilizofafanuliwa, kama hukumu za ibada na miamala, Ya pili: Elimu ya dini ya Mwenyezi Mungu Mtukufu moja kwa moja, inayo kusanya misingi ya imani na sheria za uislamu na kujua halali na haramu na tabia na adabu.