عَنْ عُبَادَةَ بْنِ الصَّامِتِ رضي الله عنه أَنَّ رَسُولَ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ قَالَ:
«لَا صَلَاةَ لِمَنْ لَمْ يَقْرَأْ بِفَاتِحَةِ الكِتَابِ».

[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Ubaada bin Swaamit -Radhi za Allah ziwe juu yake- hakika Mtume -Rehema na amani za Allah ziwe juu yake alisema:
"Hana swala yeyote ambaye hakusoma sura kifunguzi cha kitabu (suratul faatiha)".

Sahihi - Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim

Ufafanuzi

Amebainisha Mtume rehema na amani ziwe juu yake kuwa sala haikubaliki isipokuwa kwa kusoma suratul Fatiha, nayo ni nguzo miongoni mwa nguzo za swala, katika kila rakaa.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Haikubaliki kusoma sura isiyokuwa suratul Fatiha ikiwa ana uwezo wa kuisoma.
  2. Kuharibika kwa rakaa ambayo haikusomwa ndani yake suratul fatiha, kwa mwenye kufanya kusudi na mjinga na aliyesahau; kwa sababu ni nguzo, na nguzo huwa hazidondoki kwa hali yoyote ile.
  3. Kisoma cha Suratul Fatiha kinaondoka kwa maamuma anapomkuta imam karukuu.