عن أُمِّ عَطِيَّةَ رَضي الله عنها، وكَانَتْ بايَعَت النبيَّ صلى الله عليه وسلم، قالت:
كُنَّا لا نَعُدّ الكُدرَةَ والصُّفْرَةَ بعدَ الطُّهرِ شيئًا.

[صحيح] - [رواه أبو داود بهذا اللفظ، ورواه البخاري بدون زيادة (بعد الطهر)]
المزيــد ...

Kutoka kwa mama Atwiya radhi za Allah ziwe juu yake, na alikuwa kampa ahadi ya utiifu Mtume rehema na amani ziwe juu yake, amesema:
"Tulikuwa hatuchukulii maji maji ya kahawia na njano baada ya twahara kuwa ni chochote".

Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy kwa mfano wake

Ufafanuzi

Ameeleza swahaba mama Atwiya radhi za Allah ziwe juu yake kuwa wanawake katika zama za Mtume rehema na amani ziwe juu yake walikuwa hawayazingatii maji maji yanayotoka katika tupu -ambayo yanaelekea katika weusi, au katika njano- baada ya kuona twahara ya kutoka katika hedhi: kuwa ni hedhi, hawaachi swala na swaumu kwa sababu yake.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kitagalogi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Pashto Kiassam السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Maji maji yanayoshuka kutoka katika utupu wa mwanamke baada ya twahara ya hedhi hayazingatiwi hata kama yatakuwa na rangi ya kahawia au njano inayotokana na damu.
  2. Kushuka kwa maji maji ya kahawia au njano wakati wa hedhi na ada inazingatiwa kuwa ni hedhi; kwa sababu kwa wakati huo ni damu, ila tu inakuwa imechanganyikana na maji.
  3. Mwanamke haachi swala wala swaumu kwa sababu ya maji maji ya kahawia au ya njano yanayotoka baada ya twahara, bali atatawadha na ataswali.