عن بريدة بن الحصيب رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «من تَرَكَ صلاةَ العصرِ فقد حَبِطَ عَمَلُهُ».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...

Kutoka kwa Buraida bin Haswib- Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Allah- Rehma na amani ziwe juu yake- "Atakayeacha swala ya Laasiri itakuwa imeporomoka amali yake".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy

Ufafanuzi

Hadithi inaonyesha adhabu ya mwenye kuacha swala ya Alaasiri kwa makusudi, na imetajwa alaasiri kwasababu ndio swala inayodhaniwa kucheleweshwa kwasababu ya kuchoka kutokana na shughuli za mchana; na kwasababu kuikosa ni kubaya mno kuliko kukosa swala zinginezo; kwakuwa kwake ni swala ya kati kati ambayo imetajwa maalumu katika amri ya kuihifadhi katika kauli yake Mtukufu: "Zihifadhini swala na swala ya kati kati" [Al-Baqara: 238] na adhabu inayofungamana na hilo ni kuporomoka kwa amali ya mwenye kuiacha, kwa kubatilika thawabu zake, na imesemekana: makusudio ya mwenye kuiacha; atakayeiacha na akalihalalisha hilo, au akapinga uwajibu wake, inakuwa makusudio ya kuporomoka amali hapa ni kukufuru, na wametoa ushahidi kwa hili baadhi ya wanachuoni kuwa atakayeacha swala ya Alaasiri kakufuru; kwasababu hayaporomoki matendo ispokuwa kwa kuritadi, na inasemekana kuwa: limekuja katika njia ya kutia uzito; Yaani: Atakayeacha swala ya Laasiri itakuwa ni kama yameporomoka matendo yake, na huu ni katika ubora maalumu wa swala ya Laasir kuwa atakayeiacha yatakuwa yameporomoka matendo yake; kwasababu ni tukufu.

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya kifaransa Kiispania Kituruki Lugha ya Kiurdu Lugha ya Kiindonesia Lugha ya Kibosnia Lugha ya Kirashia Kibangali Kichina Kifursi Kihindi Kivetenamu Kisin-hala Ki ighori Kikurdi Kihausa Kireno Kimalayo Kitelguu Kunakili kumbukumbu mahala pa kutafsiri Burmese Thai German Kijapani Pashto Kiassam Albanian السويدية الأمهرية الهولندية الغوجاراتية الدرية
Kuonyesha Tarjama

Katika Faida za Hadithi

  1. Kuhimizwa juu ya kuihifadhi swala ya Laasiri katika wakati wake.
  2. Uharamu wa kuacha swala, na hasa hasa swala ya Laasiri.
  3. Atakayeacha swala ya Laasiri kwa makusudi basi yatakuwa yamebatilika malipo yake, na kigezo cha makusudi kimethibiti katika riwaya sahihi.