عن بريدة بن الحصيب رضي الله عنه قال: قال رسول الله صلى الله عليه وسلم : «من تَرَكَ صلاةَ العصرِ فقد حَبِطَ عَمَلُهُ».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Buraida bin Haswib- Radhi za Allah ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Allah- Rehma na amani ziwe juu yake- "Atakayeacha swala ya Laasiri itakuwa imeporomoka amali yake".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Hadithi inaonyesha adhabu ya mwenye kuacha swala ya Alaasiri kwa makusudi, na imetajwa alaasiri kwasababu ndio swala inayodhaniwa kucheleweshwa kwasababu ya kuchoka kutokana na shughuli za mchana; na kwasababu kuikosa ni kubaya mno kuliko kukosa swala zinginezo; kwakuwa kwake ni swala ya kati kati ambayo imetajwa maalumu katika amri ya kuihifadhi katika kauli yake Mtukufu: "Zihifadhini swala na swala ya kati kati" [Al-Baqara: 238] na adhabu inayofungamana na hilo ni kuporomoka kwa amali ya mwenye kuiacha, kwa kubatilika thawabu zake, na imesemekana: makusudio ya mwenye kuiacha; atakayeiacha na akalihalalisha hilo, au akapinga uwajibu wake, inakuwa makusudio ya kuporomoka amali hapa ni kukufuru, na wametoa ushahidi kwa hili baadhi ya wanachuoni kuwa atakayeacha swala ya Alaasiri kakufuru; kwasababu hayaporomoki matendo ispokuwa kwa kuritadi, na inasemekana kuwa: limekuja katika njia ya kutia uzito; Yaani: Atakayeacha swala ya Laasiri itakuwa ni kama yameporomoka matendo yake, na huu ni katika ubora maalumu wa swala ya Laasir kuwa atakayeiacha yatakuwa yameporomoka matendo yake; kwasababu ni tukufu.