عن عبد الله بن عمرو بن العاص رضي الله عنهما عن النبي صلى الله عليه وسلم قال: «ليس الواصل بالمُكَافِئِ ، ولكنَّ الواصل الذي إذا قَطعت رحِمه وصَلَها».
[صحيح] - [رواه البخاري]
المزيــد ...
Kutoka kwa Abdillaahi bin Amri bin Aaswi -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yao- Kutoka kwa Mtume rehema na Amani ziwe juu yake- Amesema: "Muunga udugu siyo mlipizaji, lakini muuunga udugu ni yule ambaye unapovunjwa udugu wake anauunga".
Sahihi - Imepokelewa na Al-Bukhaariy
Maana ya kauli yake Rehema na Amani zimfikie: "Muunga udugu si mlipizaji" Yaani: si mwanadamu aliyekamilika katika kuunga udugu kwa ndugu wa karibu ni yule mtu anayelipa wema kwa wema, bali muungaji hakika na aliyekamilika katika kuunga udugu ni yule ambaye ukikatwa udugu wake anauunga, hata kama watamfanyia ubaya, kisha analipa ubaya kwa kuwafanyia wema, huyu ndiye muungaji wa kweli, ni juu ya kila mtu kusubiri na kutaraji malipo juu ya maudhi ya ndugu zake wa karibu na jirani zake na jamaa zake na wengineo, basi hatoacha kuendelea kupata msaada kutoka kwa Mwenyezi Mungu, naye ndiye aliyepata faida, na wao ndio wenye hasara. Na kuunga udugu kunakuwa kwa mali na kwa kuwasaidia wakati wa shida, na kuondoa madhara, na kuwa na uso mkunjufu kwao na kuwaombea, na maana ya kiujumla ni kufikisha yote yanayowezekana katika mambo ya kheri, na kuzuia yote yanayowezekana katika mambo ya shari kwa kadiri ya uwezo, na umesisitiza uislamu mara nyingi juu ya kuunga udugu, ispokuwa haihesabiki ni kukata udugu kwa atakayeacha kuunga udugu kwa kuwahama kwa tahadhari au kuwakemea; kama atakayeona kuna maslahi katika kuacha kuunga udugu kwa kutaraji kuwa udugu utarudi katika hali nzuri zaidi na ya kweli, na kuacha mambo yaliyokatazwa na dini, au akahofia nafsi yake na familia yake nakuwa yeye endapo ataunga udugu na wao wakiwa wako katika mambo hayo yanayokwenda kinyume na sheria, huenda ugonjwa ukahamia kwake na kwa wale waliochini yake.