+ -

عَنْ أَنَسِ بْنِ مَالِكٍ رَضِيَ اللَّهُ عَنْهُ قَالَ: قَالَ رَسُولُ اللَّهِ صَلَّى اللهُ عَلَيْهِ وَسَلَّمَ:
«انْصُرْ أَخَاكَ ظَالِمًا أَوْ مَظْلُومًا». فَقَالَ رَجُلٌ: يَا رَسُولَ اللَّهِ، أَنْصُرُهُ إِذَا كَانَ مَظْلُومًا، أَفَرَأَيْتَ إِذَا كَانَ ظَالِمًا كَيْفَ أَنْصُرُهُ؟ قَالَ: « تَحْجُزُهُ -أَوْ تَمْنَعُهُ- مِنَ الظُّلْمِ؛ فَإِنَّ ذَلِكَ نَصْرُهُ».

[صحيح] - [رواه البخاري] - [صحيح البخاري: 6952]
المزيــد ...

Imepokewa kutoka kwa Anas bin Maliki -radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- amesema: Amesema Mtume wa Mwenyezi Mungu -rehema na amani ziwe juu yake:
"Msaidie ndugu yako akiwa amedhulumu au kudhulumiwa", Akasema mtu mmoja: Ewe Mtume wa Mwenyezi Mungu, unaonaje ikiwa ndugu yangu kadhulumu, vipi nitamsaidia? Akasema: "Unamuhama au unamzuia asifanye dhulma, kwa kufanya hivyo ndiyo kumnusuru".

[Sahihi] - [Imepokelewa na Al-Bukhaariy] - [صحيح البخاري - 6952]

Ufafanuzi

Mtume rehema na amani ziwe juu yake amemuamrisha Muislamu kumsadia ndugu yake Muislamu sawa sawa awe kadhulumu au kadhulumiwa, mtu mmoja akasema: Ewe Mjumbe wa Mwenyezi Mungu, nimnusuru atakapokuwa emedhulumiwa kwa kumuondolea dhuluma, wasemaje ikiwa kadhulumu nitamsaidia vipi? Akasema: Utamzuia, na kumshika mkono na umkinge na umzuie na dhuluma; kwa kufanya hivyo ndiko kumnusuru dhidi ya Shetani wake na nafsi yake yenye kuamrisha maovu.

Katika Faida za Hadithi

  1. Hapa kuna tahadhari juu ya haki miongoni mwa haki za udugu wa kiimani baina ya Waislamu.
  2. Kumzuia dhalimu, na kumkataza dhidi ya dhuluma.
  3. Uislamu unakwenda kinyume na uelewa wa zama za ujinga, kiasi ambacho walikuwa wakisaidizana sawa sawa wawe wamedhulumiwa wao wamemdhulumu mwingine.
Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kiassam الرومانية المجرية الجورجية
Kuonyesha Tarjama