+ -

عن عائشة رضي الله عنها قالت: تُوُفِّيَ رسول الله صلى الله عليه وسلم وما في بيتي من شيء يَأكُلُهُ ذُو كَبدٍ إلا شَطْرُ شَعير في رَفٍّ لي، فأكَلتُ منه حتى طال عليَّ، فَكِلْتُهُ فَفَنِيَ.
[صحيح] - [متفق عليه]
المزيــد ...

Kutoka kwa Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- Amesema: Alifariki Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- hali yakuwa hakuna chochote nyumbani kwake anachoweza kukila mwenye ini (uhai) ila kiasi kidogo cha ngano kilichokuwa katika ubao wangu (wa kuhifadhia chakula), nikala mpaka kikakaa muda mrefu, nilipokipima kikamalizika
[Sahihi] - [Wamekubaliana Bukhaariy na Muslim]

Ufafanuzi

Anaeleza Aisha -Radhi za Mwenyezi Mungu ziwe juu yake- kuwa Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- alifariki hali yakuwa hakuna nyumbani kwake chochote isipokuwa kiasi kidogo cha ngano, na maana yake ni kiwango kidogo cha ngano, kama alivyoifasiri imamu Tirmidhiy, akaendelea kula katika chakula alichokiacha Mtume -Rehema na Amani ziwe juu yake- kwa muda mrefu, alipokipima kikamalizika, na hii ni ishara ya kuendelea kwa baraka zake -Rehema na Amani ziwe juu yake- katika chakula hicho kidogo, pamoja na kutokuwepo kwa kipimo kinachoonyesha kiasi wakati wa kumtegemea Mwenyezi Mungu, kipimo wakati wa kuuziana kinahitajika kwaajili ya kuweka sawa haki ya wale wenye kuuziana, ama kipimo wakati wa kutoa sadaka haipendezi (si katika sunna).

Tafsiri: Lugha ya kiingereza Lugha ya Kiurdu Kiispania Lugha ya Kiindonesia Kibangali Lugha ya kifaransa Kituruki Lugha ya Kirashia Lugha ya Kibosnia Kisin-hala Kihindi Kichina Kifursi Kivetenamu Kitagalogi Kikurdi Kihausa Kireno
Kuonyesha Tarjama